Posts

Showing posts from October, 2025

MGOMBEA MWENZA WA URAIS KUPITIA (CCM) BALOZI NCHIMBI ASHIRIKI ZOEZI LA KUPIGA KURA

Image
Mgombea mwenza wa Urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi akishiriki zoezi la kupiga kura ya kumchagua Rais,Mbunge na Diwani katika mtaa wake, eneo la Kilimani, jijini Dodoma leo tarehe 29, Oktoba 2025.

WAPIGA KURA WAJITOKEZA KWA WINGI KATA YA KIRUMBA, ILEMELA – MWANZA

Image
Zoezi la kupiga kura linaendelea kwa hali ya utulivu katika Kata ya Kirumba, Halmashauri ya Ilemela, jijini Mwanza, huku wananchi wakijitokeza kwa wingi kutekeleza haki yao ya kikatiba. Wananchi wameonekana wakiwa katika mistari wakiingia vituoni mapema asubuhi, wakisubiri kwa utulivu nafasi yao ya kupiga kura. Maafisa wa Tume ya Uchaguzi wamesema maandalizi yamekuwa mazuri na vifaa vyote vya kupigia kura vimefika kwa wakati. Wamewataka wapiga kura kuendelea kujitokeza kwa amani na kufuata maelekezo yanayotolewa na wasimamizi wa vituo, ili kuhakikisha zoezi hilo muhimu kwa demokrasia ya nchi linafanikiwa kwa utulivu na uwazi.

MAKAMU WA RAIS DKT PHILIP MPANGO ASHIRIKI ZOEZI LA KUPIGA KURA KIGOMA

Image
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akishiriki zoezi la kupiga kura ya kuchagua Rais, Mbunge na Diwani akiwa katika Kijiji cha Kasumo, Wilaya ya Buhigwe mkoani Kigoma leo tarehe 29 Oktoba 2025.

DKT. MWINYI APIGA KURA MJINI MAGHARIBI

Image
Mgombea wa nafasi ya Urais wa Zanzibar kupitia tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Hussein Ali Mwinyi akishiriki katika zoezi la upigaji wa kura katika Kituo cha kupigia Kura cha Kariakoo kilichopo Wilaya ya Mjini, Mkoa wa Mjini Magharibi leo Jumatano Oktoba 29, 2025.

MIONDOMBINU YA BARABARA YAIMARIKA SONGEA, WAKULIMA WAFAIDIKA NA UjenYzi WA BARABARA NA MADARAJA*

Image
#Wananchi wa Mkongotema waepukana na Daraja la miti Songea, Ruvuma Serikali imetoa kiasi cha shilingi milioni 900 kwa ajili ya kuondoa vikwazo katika Barabara wilayani Songea kwa ujenzi wa daraja la Mto Lumecha na kufungua barabara ya kilomita 4 katika kata ya Mkongotema sambamba na ujenzi wa daraja la Mto Liweta iliyopo katika Kata ya Mpandangindo. Meneja wa Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) wilayani humo, Mhandisi Bakari John, ameeleza kuwa hizo ni juhudi za kuboresha miundombinu ya barabara zikilenga kuinua uchumi wa wakulima wa Wilaya ya Songea kupitia mradi wa RISE programu ya Uondoaji Vikwazo katika Barabara (bottleneck) iliyopo chini ya TARURA. "Wananchi wa Mkongotema na Mpandangindo, ambao ni wakulima wa mazao ya biashara kama tangawizi, mahindi na parachichi, walikuwa wakikabiliwa na changamoto ya kusafirisha mazao yao kutoka mashambani hadi sokoni".  “Kukosekana kwa miundombinu bora kulisababisha gharama za usafirishaji kuwa juu na kupunguza faida kw...

TAASISI ZA MADINI ZAELEZA MAFANIKIO ROBO YA KWANZA 2025/26*

Image
*Tume ya Madini Yakusanya Bilioni 315.4 Robo ya Kwanza* *Kilo 2,356.413 za Dhahabu Zasafishwa Kiwanda cha Mwanza Metals Refinery* *Ununuzi wa Helkopta ya Utafiti unaendelea* *Viwanda vya Kuzalisha Mkaa wa Rafiki Briquettes Mbioni Dodoma, Tabora* *TGC Yaanzisha duka la bidhaa za mapambo ya Vito, AICC-Arusha* *Dodoma* Menejimenti ya Wizara ya Madini Oktoba 27, 2025 ilikutana na Wakuu wa Taasisi zake katika kikao kilicholenga kupokea taarifa ya ufuatiliaji na tathmini kwa majukumu yaliyotekelezwa na taasisi hizo katika kipindi cha Robo ya Kwanza ya Mwaka wa Fedha 2025/26.  Taasisi zilizo chini ya Wizara ni pamoja na Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini Tanzania (GST) Shirika la Madini la Taifa (STAMICO), Tume ya Madini, Taasisi ya Uhamasishaji Uwazi na Uwajibikaji katika Rasilimali Madini, Mafuta na Gesi Asilia (TEITI) na Kituo cha Jemolojia Tanzania (TGC) cha jijini Arusha. Katika taarifa iliyowasilishwa na Tume ya Madini, ilielezwa kwamba, katika kipindi robo ya kwanza, tayari k...

MHE. CHUMI AWAHAHAKISHIA WAANGALIZI UCHAGUZI HURU

Image
Serikali imeihakikishia Timu ya Waangalizi ya Uchaguzi ya Wabunge-Wanawake kutoka Jumuiya ya Madola (CWP) kuwa Uchaguzi Mkuu wa Rais, wabunge na madiwani uliopangwa kufanyika Oktoba 29, 2025 utakuwa huru, haki na wazi. Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Cosato Chumi alipokutana na timu hiyo jijini Dodoma Oktoba 28, 2025. Mhe. Chumi alisema Serikali kupitia taasisi husika zikiwemo Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) na Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), imekamilisha maandalizi yote muhimu kuhakikisha kuwa uchaguzi huo unafanyika kwa kuzingatia Katiba ya Nchi, sheria za uchaguzi na vigezo vya kidemokrasia.  Alisema kuwa uchaguzi wa mwaka huu ni wa aina yake kutokana na kuwa jumuishi zaidi ambapo wagombea 17 wa nafasi ya Rais, watatu ni wanawake na 10 ni wagombea mwenza, huku ikishuhudiwa pia kuwa idadi kubwa ya wanawake wanawania nafasi za ubunge na udiwani katika pande zote za muungano. Naye, Kiongozi wa timu hiyo, Mhe. Ndan...

WANANCHI KATA YA KAKESIO NGORONGORO KUNUFAIKA NA MRADI WA MAJI*

Image
Wananchi wa kata ya Kakesio iliyoko Tarafa ya Ngorongoro Wilaya ya Ngorongoro Mkoani Arusha watanufaika na mradi wa Maji kwa ajili ya Mifugo na matumizi ya binadamu kufuatia Serikali kupitia Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA) kuchimba Kisima cha Maji chenye urefu wa mita 110 ambacho kinatarajiwa kuzalisha maji lita 80,000 kwa siku.                                                                 Uchimbaji wa Kisima hicho ni muendelezo wa kazi nzuri inayofanya na Serikali kwa Wananchi wanaoishi katika eneo la Hifadhi ya Ngorongoro ambapo Kisima kama hicho  kimechimbwa eneo la Mlima matiti kwa ajili ya wananchi wa Kata ya Endulen na Alaetoli na baadae mradi kama huo utatekelezwa katika Kata ya Olbalbal ili kusaidia wananchi kukabiliana na changamoto ya upungufu wa maji kwa mifugo katika msimu wote wa mwaka.

ELIMU YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA YAWAFIKIA MAAFISA DAWATI NGAZI YA MIKOA NA HALMASHAURI*

Image
📌 *Lengo ni  kuwa na uelewa wa pamoja katika utekelezaji  wa Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia.* 📌 *Mafunzo kuhusisha mikoa 26 na Halmashauri zake.* Wizara ya Nishati imeanza kutoa elimu kuhusu Nishati Safi ya Kupikia  kwa  Maafisa Dawati wa Nishati Safi ya Kupikia ngazi ya mikoa na halmashauri  kwa lengo la kuwa na uelewa wa pamoja katika utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Nishati Safi ya Kupikia pamoja na  kuwawezesha Maafisa Dawati kutambua majukumu yao katika utekelezaji wa mkakati.. Akifungua  mafunzo hayo, wilayani Kibaha mkoani Pwani,  Mwakilishi wa Katibu Tawala wa Mkoa wa  Pwani, Bi. Hadija Mruma ameipongeza Wizara ya Nishati kwa jitihada mbalimbali inazochukua kwa vitendo katika kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini mojawapo ikiwa ni kuhakikisha elimu na vifaa vya nishati safi ya kupikia vinafika hadi ngazi za Mikoa, Halmashauri na Vijiji. Ameeleza kuwa Mkoa wa Pwani unachukua hatua mbalimbali kuhakikish...

KUKAMILIKA KWA MRADI WA AGRI-CONNECT UTABADILI TASWIRA YA MIUNDOMBINU MBINGA*

Image
# Ni barabara ya Utili–Mahande itakayofungua fursa za kiuchumi kwa wakulima  #Vikundi kazi vinne vyasajiliwa  Mbinga, Ruvuma Katika juhudi za kuboresha miundombinu na kuinua uchumi wa wakazi wa wilaya ya Mbinga, Meneja wa Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) wilayani humo, Mhandisi Oscar Musa, amesema mradi wa Agri-Connect unaotekelezwa katika barabara ya Utili–Mahande umefikia hatua muhimu ya ujenzi. Mradi huo wenye urefu wa kilomita 14.4 na thamani ya shilingi bilioni 16.5 ulianza kutekelezwa mwezi Novemba 2024 na unatarajiwa kukamilika Mei 2026, ikiwa ni kipindi cha miezi 18. Kwa sasa, kazi ya kuchonga na kufungua barabara yote imekamilika, huku ujenzi wa madaraja saba ukiendelea sambamba na uwekaji wa tabaka la udongo ambapo kilomita 8 tayari zimekamilika. Mhandisi Musa amesema kwamba mradi huo unatekelezwa na Mkandarasi kutoka kampuni ya Ovans Construction Ltd iliyoko Mbinga. “Lengo kuu la mradi huu ni kuwahudumia wananchi wa vijiji vya Utili, Mahande na Mbin...

RC KILIMANJARO ATOA ONYO KALI DHIDI YA MAANDAMANO WAKATI WA UCHAGUZI.

Image
RC KILIMANJARO ATOA ONYO KALI DHIDI YA MAANDAMANO WAKATI WA UCHAGUZI. Na Musa Mathias, Same, Kilimanjaro. Subscribe Channel yetu ya Youtube hapa.  https://youtube.com/@kipeoonlinemedia?si=I4xrm3DGzDSHWbuH Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Mhe. Nurdin Babu, amewaonya vikali baadhi ya wananchi wanaopanga kufanya vurugu na maandamano mkoani humo katika kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Oktoba 29, 2025. Babu ametoa onyo hilo wakati akizungumza kwenye kongamano la wanawake wilayani Same lililofanyika katika ukumbi wa mikutano wa Nzoroko, likihudhuriwa na zaidi ya wanawake 300. Amesema Mkoa wa Kilimanjaro umejipanga kuhakikisha usalama unakuwepo kabla, wakati na baada ya uchaguzi, huku akisisitiza wananchi kujitokeza kwa wingi kupiga kura kwa amani. “Serikali ya mkoa na wilaya tumejipanga kuhakikisha ulinzi na usalama unakuwepo. Nendeni mkapige kura kwa amani. Mkoa wa Kilimanjaro si wa vurugu, wala watu wake hawataki maandamano. Wale wanaotaka kufanya maandamano watafute n...

SERIKALI YATENGA BILIONI 5.2 UJENZI WA MIUNDOMBINU MBINGA: DC MAKORI*

Image
#Mradi wa TACTIC kuleta mapinduzi makubwa #Wananchi wafurahia uwekaji taa za barabarani  Mbinga, Ruvuma Serikali kupitia Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) kwa mwaka wa fedha 2025/2026 imetenga jumla ya shilingi bilioni 5.2 kwa ajili ya maendelezo ya miundombinu ya barabara  wilayani Mbinga mkoani Ruvuma. Hayo yameelezwa na Mkuu wa Wilaya ya Mbinga, Mhe. Kisare Makori wakati akielezea  uendelezaji wa miundombinu ya barabara unaofanywa na TARURA wilayani humo. Amesema ujenzi wa barabara kupitia Wakala huo umeweza kuwasaidia wananchi kusafirisha mazao yao pamoja na kuinua uchumi katika halmashauri zote mbili za wilaya ya Mbinga. Wilaya ya Mbinga ni miongoni mwa kapu la chakula la Taifa kwani kuna uzalishaji mkubwa wa mazao ya chakula na biashara, mazao mengi ya chakula na biashara yanastawi kutokana na rutuba ya eneo hili”. “Tunaishukuru serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa jinsi ambavyo anavyoendelea kutuletea fedha kup...