Posts

Showing posts from October, 2025

CCM YABADILISHA MAISHA NAMONGE

Image
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Bukombe kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Doto Mashaka Biteko amesema kuwa Serikali ya CCM inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imebadilisha maisha ya watu wa Kata ya Namonge  kwa kuleta miradi ya maendeleo ikiwemo kufungua barabara, maji na umeme. Dkt. Biteko amesema hayo Oktoba 1, 2025 wakati wa mkutano wa kampeni katika Kijiji cha Bwenda, Kata ya Namonge wilayani Bukombe mkoani Geita ikiwa ni sehemu Kampeni za Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani utakaofanyika Oktoba 29, mwaka huu. Dkt. Biteko amesema kuwa awali Kata hiyo haikuwa na maji, umeme,barabara na hata walimu waliochaguliwa kufundisha katika shule za Kata hiyo hawakufurahia kazi zao kutokana na hali iliyokuwa. “Kituo cha afya kimekamilika, gari la kubeba wagonjwa kesho litakuwepo, leo tuna shule 14 za msingi, shule tatu za sekondari na tutataka kujenga shule zingine za kidato cha tano na sita,” amesema Dkt. Biteko. Ameendelea kusema ikiwa wananchi hao wanahitaji mae...

RAHA YA UHIFADHI NI KUISHI VIZURI NA MAJIRANI

Image
Na mwandishi wetu  Naibu Kamishna wa Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro anayesimamia Uhifadhi,Utalii na Maendeleo ya Jamii   Joas Makwati Oktoba 1 mwaka 2025 ameongoza kikao cha ujirani mwema na viongozi wa maeneo  ya vijiji vya jirani na kusisitiza umuhimu wa ushirikiano ili kujenga mazingira mazuri ya kufanya kazi pamoja. Katika kikao hicho pamoja na watendaji wengine Naibu Kamishna aliongozana na Kamishna Msaidizi Mwandamizi  anayeshughulikia maendeleo ya jamii Bi. Gloria Bideberi ambapo viongozi wote walikubaliana  kufanya kazi kwa pamoja. Viongozi wa vijiji  wa wilaya ya Karatu na Monduli walieleza changamoto kubwa zinazowakabili wananchi, ikiwemo kupoteza mazao kutokana na uvamizi wa wanyama pori kama tembo na nyati wanaoingia katika makazi na mashamba, hali inayohatarisha shughuli za kiuchumi za kaya nyingi zinazotegemea kilimo. Naibu Kamishna Joas Makwati alieleza kuwa  pamoja na suala zima la ujirani mwema kikao hicho  kitasaidia kuwek...

WAZIRI KOMBO AWASILI ZIMBABWE KUSHIRIKI MKUTANO WA 22 WA MAWAZIRI WA MAMBO YA NJE WA AFRIKA NA NORDIC

Image
Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo, amewasili jijini Victoria Falls, Zimbabwe, kushiriki Mkutano wa 22 wa Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Afrika na Nordic, unaofanyika kuanzia tarehe 2 hadi 3 Oktoba, 2025. Akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Victoria Falls Mhe. Waziri Kombo amepokelewa na Balozi wa Tanzania nchini Zimbabwe, Mhe. CP Suzan S. Kaganda, pamoja na viongozi wa ngazi ya juu kutoka Tanzania na Zimbabwe. Ziara yake inafanyika kufuatia mwaliko rasmi kutoka kwa Waziri wa Mambo ya Nje na Biashara za Kimataifa wa Jamhuri ya Zimbabwe, Mhe. Prof. Dkt. Amon Murwira. Mkutano wa mwaka huu unaongozwa na kaulimbiu isemayo: “Innovation for Impact: Leveraging Technology and Collaboration for Future-Ready Societies” (Ubunifu kwa Matokeo: Kutumia Teknolojia na Ushirikiano kwa Jamii Zinazojitayarisha kwa Baadaye). Kaulimbiu hii inalenga kusisitiza umuhimu wa ubunifu, teknolojia na mshikamano wa kimataifa katika kujenga jamii imar...