*MHE. SALOME AHAMASISHA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA KUPITIA MARATHON*
Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, leo Juni 27, 2026 ameshiriki Mbio za Nishati Safi ya Kupikia (Clean Cooking Marathon) zilizofanyika katika Viwanja vya St. Peters Oysterbay jijini Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya kampeni ya kitaifa ya kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini. Akizungumza wakati wa kufungua mbio hizo, Mhe. Salome amesema pamoja na hatua nzuri iliyofikiwa, matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini bado yako katika kiwango cha asilimia 28.6, hali inayoonesha kuwa bado kuna kazi kubwa ya kufanya ili kufikia lengo la asilimia 80 ya matumizi ya nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034. Amesema mbio hizo si mashindano ya kawaida ya kutafuta medali au vikombe, bali ni chachu ya mabadiliko ya kifikra na kijamii yanayolenga kulinda afya za wananchi, kuhifadhi mazingira na kuwawezesha wananchi kiuchumi, huku akisisitiza kuwa Serikali itaendelea kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia wa mwaka 2024–2034 unaolenga kuhakikish...