Posts

Showing posts from February, 2025

RAIS MWINYI:SERIKALI INAENDELEA KUWEKEZA KATIKA ELIMU YA JUU.

Image
  RAIS MWINYI:SERIKALI INAENDELEA KUWEKEZA KATIKA ELIMU YA JUU. Rais wa  Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt, Hussein Ali Mwinyi amesema Serikali Ina Wajibu Mkubwa wa Kuendelea Kuwekeza katika Elimu ya juu ili kuzalisha Wataalamu wengi zaidi watakaochangia Maendeleo katika Sekta tofauti na Ustawi wa Wananchi. Rais Dkt.Mwinyi amesema hayo alipomuwakilisha  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt, Samia Suluhu  Hassan katika  Kongamano la Kumuenzi Mkuu  wa Kwanza wa Chuo Kikuu cha Afya na  Sayansi Shirikishi Tawi la Muhimbili  (MUHAS) Rais wa Awamu ya Pili ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Hayati Ali Hassan Mwinyi na Uwekaji wa Jiwe la Msingi wa Ujenzi wa Ndaki ya Chuo hicho  jijini Dar es Salaam. Aidha, Rais Dkt.Mwinyi amesema Serikali inathamini Mafanikio Makubwa yaliofikiwa na Chuo cha Muhas  tangu kuanzishwa kwake  yanayochangia kuzalisha Wataalamu katika Sekta ya Elimu, Afya, Ufanyaji wa Tafiti na Utoaji wa...

DC SAME AELEKEZA WANANCHI WASIO KUWA NA VYOO KUCHUKULIWA HATUA SAME

Image
DC SAME AELEKEZA WANANCHI WASIO KUWA NA VYOO KUCHUKULIWA HATUA. Same, Kilimanjaro.  Maafisa afya, Walimu pamoja na watendaji wa kata na vijiji ndani ya Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, wamesisitizwa kufanya ukaguzi wa kila kaya na kuchukua hatua za kisheria kwa kaya zisizokuwa na vyoo. Lengo ni kuendelea kuhamasisha na kutoa elimu kwa wananchi juu ya usafi wa mazingira na matumizi bora ya vyoo ili kuepuka magonjwa ya mlipuko. Wito huo umetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Same, Mhe. Kasilda Mgeni, wakati wa kikao cha Kamati ya Afya ya Msingi wilayani Same. Amesema kuwa elimu na uhamasishaji kwa wananchi kuhusu usafi wa mazingira na matumizi ya vyoo ni muhimu kwa afya ya jamii na kuzuia magonjwa yanayotokana na uchafu (Magonjwa ya mlipuko). "Niendelee kusisitiza walimu, maafisa afya pamoja na watendaji wa kata na vijiji kufanya ukaguzi wa kila nyumba na kuwachukulia hatua wale watakaobainika kutokuwa na vyoo, Pia utoaji wa elimu kwa wananchi pamoja na uhamasishaji wa matumizi ya vyoo n...

MKUU WA WILAYA YA SAME AKERWA NA USIMAMIZI MBOVU WA MRADI WA MAJI WA RUWASA KATA YA KISIWANI.

Image
MKUU WA WILAYA YA SAME AKERWA NA USIMAMIZI MBOVU WA MRADI WA MAJI Mkuu wa Wilaya ya Same, Mhe. Kasilda Mgeni, ameonesha kukerwa na usimamizi wa mradi wa maji unaotekelezwa na Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA) katika Kata ya Kisiwani, wilayani humo. Licha ya serikali kutoa shilingi milioni 720 kwa ajili ya mradi huo, bado haujanufaisha walengwa, huku ikidaiwa kuwa baadhi ya wananchi wamejiunganishia maji kinyemela. Hali hiyo imebainika wakati wa kikao na wananchi wa kijiji cha Kisiwani Barazani kilichopo kata ya Kisiwani ambapo msimamizi wa mradi alishindwa kutoa maelezo ya maswali yaliyoulizwa kaktika mkutano huo kuhusu gharama za mradi, idadi ya walengwa, na hatua zilizochukuliwa dhidi ya waliojiunganishia maji kinyemela. Kushindwa kwake kujibu maswali hayo kuliibua maswali mengi mbele ya Mkuu wa Wilaya, Kamati ya Usalama ya Wilaya, Mkurugenzi wa Halmashauri, wataalamu, na wananchi waliohudhuria mkutano huo. Mhe. Kasilda Mgeni alieleza kutoridhishwa na hali hiyo, ...

OPARESHENI YA KUWADHIBITI FISI SIMIYU YAONESHA MAFANIKIO MAKUBWA

Image
OPARESHENI YA KUWADHIBITI FISI SIMIYU YAONESHA MAFANIKIO MAKUBWA Simiyu . Oparesheni maalumu ya kuwadhibiti wanyamapori wakali na waharibifu aina ya fisi waliokuwa wanaleta taharuki na madhara Kwa jamii inayoendelea Mkoani Simiyu imeonesha mafanikio makubwa baada ya fisi 16 kuvunwa ikiwa ni hatua muhimu iliyochukuliwa na Serikali kupitia Wizara ya Maliasili na Utalii ya kuhakikisha usalama na utulivu Kwa wananchi vinarejea. Hayo yamesemwa leo Februari 19, 2025 na Mkuu wa Mkoa wa Simiyu Mhe. Kenani Kihongosi alipokuwa akiongea na waandishi wa vyombo mbalimbali vya habari. Mhe. Kihongosi amesema kufuatia changamoto hiyo,  Serikali ilichukua jukumu kubwa la kuhakikisha inalinda wananchi wake ikiwemo kuanzisha oparesheni maalumu inayohusisha Jeshi la Uhifadhi Kwa Taasisi za TAWA, TANAPA na TFS Kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi pamoja na wananchi, oparesheni inayotajwa kuanza  Januari 25, 2025. "Tarehe 20/12/2024 baada ya fisi kuvamia wananchi Serikali ilichukua hatua kubwa ya ku...

Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji Wilayani Same Watakiwa Kufanya Kazi kwa Uwazi na Kuzingatia Sheria

Image
WENYEVITI WA VIJIJI NA VITONGOJI WILAYANI SAME WATAKIWA KUFANYA KAZI KWA UWAZI NA KUZINGATIA SHERIA. Same, Kilimanjaro.  Wenyeviti wa vijiji na vitongoji wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, wametakiwa kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia sheria, taratibu na miongozo. Aidha, wamehimizwa kusimamia kwa uwazi mapato na matumizi ya vijiji vyao, kutoa taarifa za miradi inayotekelezwa, na kuhakikisha wanashughulikia kero na malalamiko ya wananchi kwa ufanisi ili kuimarisha utawala bora. Mkuu wa Wilaya ya Same, Mhe. Kasilda Mgeni, ametoa wito huo wakati wa mafunzo maalumu kwa wenyeviti wa vijiji na vitongoji, yanayofanyika wilayani humo kwa muda wa siku mbili. Mafunzo haya yanalenga kuwaongezea viongozi hao uelewa na uwezo, kujua majukumu yao ya utendaji na ya msingi kama wenyeviti wa vijiji na vitongoji ili kuongoza kwa ufanisi zaidi. Mhe. Kasilda amewataka wenyeviti hao pia kuhakikisha usalama wa mipaka ya maeneo yao kwa kuzuia uhamiaji holela wa wananchi wanaoingia bila utaratibu kwa ...

MKUU WA WILAYA YA SAME AWATAKA WASIMAMIZI WA MIRADI KUTOA USHIRIKIANO KWA MAAFISA WA SERIKALI.

Image
MKUU WA WILAYA YA SAME AWATAKA WASIMAMIZI WA MIRADI KUTOA USHIRIKIANO KWA MAAFISA WA SERIKALI. Same, Kilimanjaro.  Mkuu wa Wilaya ya Same, Mhe. Kasilda Mgeni, amewataka wasimamizi wa miradi inayoendelea kujengwa ndani ya wilaya hiyo kushirikiana na maafisa wa serikali wanapofanya ziara za ukaguzi. Amesisitiza kuwa ziara hizo zina lengo la kuhakikisha miradi inatekelezwa kwa kuzingatia ubora, thamani ya fedha, na kasi inayotakiwa ili kuepusha ubadhilifu na ujenzi wa majengo yasiyo na viwango stahiki. Mhe. Kasilda alitoa kauli hiyo alipokuwa akikagua ujenzi wa shule mpya ya sekondari ya Kata ya Hedaru, katika ziara hiyo aliambatana na kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya ya Same ambapo Alibainisha kuwa maafisa wa serikali na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi ya Wilaya wanapokagua miradi, wanakuwa na nia njema ya kushauri na kuhakikisha kuwa miradi inatekelezwa kwa viwango vilivyokusudiwa. Mkuu wa wilaya ya Same Mhe Kasilda Mgeni akijaza udongo kwenye ndoo kitendo kinachoonesha ushiriki ka...

USIKU WA WAPENDANAO WAFANA HIFADHI YA TAIFA YA MILIMA UDZUNGWA

Image
  USIKU WA WAPENDANAO WAFANA HIFADHI YA TAIFA YA MILIMA UDZUNGWA Na Musa Mathias Njogolo Mikumi, Morogoro.  Watanzania kutoka maeneo mbalimbali ya nchi wamejitokeza kwa wingi kutembelea Hifadhi ya Taifa ya Milima Udzungwa kusherehekea Sikukuu ya Wapendanao, Februari 14. Tukio hilo ni sehemu ya kuhamasisha utalii wa ndani na kuunga mkono juhudi za serikali ya awamu ya sita ya ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, inayoongozwa na Dkt. Samia Suluhu Hassan , katika kukuza sekta ya utalii kupitia kampeni mbalimbali.  Akizungumza kwa niaba ya Kamanda wa Kanda ya Mashariki wakati wa hafla maalum ya kuwapokea wageni hao, Kamishna Msaidizi wa Uhifadhi Kanda ya Mashariki TANAPA, Fredrick Malisa, aliwapongeza Watanzania kwa mwitikio wao mkubwa wa kutembelea vivutio vya utalii nchini, akisema kuwa hatua hiyo ni ya kizalendo na inachangia kukuza uchumi wa taifa kupitia sekta ya utalii. "Ni jambo la kufurahisha kuona Watanzania wakizidi kutambua thamani ya rasilimali za Nchi yao kwa kuj...

MKUU WA WILAYA YA SAME AAGIZA TAASISI ZA SERIKALI ZINAZOKUSANYA MAPATO KUBORESHA NA KUBUNI VYANZO VIPYA VYA MAPATO.

Image
  MKUU WA WILAYA YA SAME AAGIZA TAASISI ZA SERIKALI ZINAZOKUSANYA MAPATO KUBORESHA NA KUBUNI VYANZO VIPYA VYA MAPATO. Same, Kilimanjaro.  Mkuu wa Wilaya ya Same, Mhe. Kasilda Mgeni, amezitaka taasisi za serikali zinazokusanya mapato kupitia utoaji wa huduma mbalimbali kwa wananchi ndani ya kubuni vyanzo vipya vya mapato ili kuimarisha uwezo wao wa kifedha na kufanikisha malengo ya ukusanyaji wa mapato waliyojiwekea. Taasisi hizo ni Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Wakala wa Maji na Usafi wa Mazingira Vijijini (RUWASA), Mamlaka ya Maji Same Mwanga (SAMWASA), Hifadhi ya Taifa Mkomazi, Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS), Halmashauri ya Wilaya ya Same pamoja na kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya.  Akizungumza katika kikao cha mapato ambacho kimewakutanisha Halmashauri ya Wilaya ya Same, wakuu wa taasisi za serikali ndani ya wilaya hiyo katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Same, Mhe. Kasilda Mgeni amesisitiza umuhimu wa kuboresha vyanzo vya mapato...

TAWA YAKABIDHI MADAWATI 295 KWA SHULE ZA MKOA WA SIMIYU.

Image
TAWA YAKABIDHI MADAWATI 295 KWA SHULE ZA MKOA WA SIMIYU. Na Mwandishi Wetu. SERIKALI kupitia Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania - TAWA imekabidhi madawati 295 yenye thamani ya Shillingi Millioni 25.9 Kwa shule za sekondari na msingi Mkoani Simiyu hatua inayolenga kuboresha mazingira ya elimu kwa shule zinazozunguka Pori la Akiba Maswa kama sehemu ya ujirani mwema kati ya TAWA na jamii.  Akizungumza na waandishi wa habari Februari 7, 2025 mkoani humo Afisa Habari wa TAWA Beatus Maganja amesema TAWA Kwa kushirikiana na Kampuni ya uwindaji wa kitalii BUSHMAN SAFARI TRACKERS wametoa madawati 295, meza (2) na viti viwili (2) Kwa shule za msingi na sekondari zilizopo wilaya za Itilima na Bariadi ambapo wilaya ya Itilima imepata madawati 190, meza 1 na kiti kimoja (1) na wilaya ya Bariadi imepata madawati 105, meza 1 na Kiti kimoja (1). Maganja amesema TAWA imekuwa na utaratibu wa kurejesha faida zinazotokana na shughuli za uhifadhi kwa jamii zinazozunguka maeneo ya hifadhi zi...

MKUU WA WILAYA YA SAME AKUTANA NA WADAU WA BIASHARA YA MBAO KUJADILI MAENDELEO NA CHANGAMOTO.

Image
  MKUU WA WILAYA YA SAME AKUTANA NA WADAU WA BIASHARA YA MBAO KUJADILI MAENDELEO NA CHANGAMOTO. Same, Kilimanjaro.  Mkuu wa Wilaya ya Same, Mhe. Kasilda Mgeni, amekutana na wadau wa biashara ya mbao kujadili maendeleo na changamoto zinazowakumba ili ziweze kutatuliwa kwa lengo la kuboresha mazingira ya biashara na kukuza uchumi wa wilaya. Kikao hicho kimefanyika leo, Februari 6, katika ukumbi wa mikutano wa ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Same. Kimewakutanisha wadau mbalimbali wilayani humo, wakiwemo Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Mamlaka ya Uhifadhi wa Misitu Tanzania (TFS), pamoja na viongozi wengine wa serikali. Akizungumza katika kikao hicho, Mhe. Kasilda amesisitiza kuwa dhamira ya serikali ni kuhakikisha biashara ndani ya wilaya inastawi. (Picha: Mkuu wa Wilaya ya Same Mhe. Kasilda Mgeni akizungumza katika kikao cha wadau wa biashara ya mbao), Picha na Musa Mathias.  "Wafanyabiashara wa mbao ni wadau muhimu, na serikali inawatambua kupitia kodi wanazolipa. Ni lazima t...