Posts

Showing posts from April, 2025

DKT. BITEKO ALITAKA SHIRIKA LA MAENDELEO YA PETROLI KUONGEZA KASI YA UENDELEZAJI VITALU VYA MAFUTA NA GESI ASILIA*

Image
📌 *Asema lengo ni kuendelea kuwa na uhakika wa usalama wa nishati nchini* 📌 *Azindua Mkakati wa Kwanza wa Muda mrefu wa Shirika (2025-2050)* 📌 *Asisitiza Jamii zinazozunguka miradi ya Mafuta na Gesi Asilia kutopuuzwa* 📌 *Apongeza Bodi na Menejimenti ya TPDC kwa kuipambanua Tanzania kama kitovu cha Mafuta na Gesi Asilia* 📌 *Balozi Sefue asema Mpango  unakusudia kuongeza matumizi ya Gesi Asilia kutoka matumizi ya kawaida* Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko ameliagiza Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC)  kuongeza kasi ya uendelezaji wa Vitalu vya utafutaji wa Mafuta na Gesi Asilia ikiwemo Mnazi Bay Kaskazini, Eyasi Wembere, Songo Songo Magharibi na Mradi wa Kuchakata na Kusindika Gesi Asilia (LNG) ili nchi iendelee kuwa na uhakika wa upatikanaji wa nishati kwa ajili ya soko la ndani na nje. Ameyasema hayo leo jijini Dodoma wakati akizindua Mkakati wa Muda Mrefu wa Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) wa miaka 25 (2024/25 hadi...

TIJA KWA NCHI NDIYO KIPAUMBELE CHA UTEKELEZAJI WA MRADI WA KUCHAKATA NA KUSINDIKA GESI ASILIA (LNG)- DKT.BITEKO*

Image
📌 *Asema kiu ya Serikali ni kuona mradi unatekelezwa ila maslahi ya Taifa ndiyo kipaumbele* 📌 *Alieleza Bunge hatua zinazochukuliwa na Serikali kuhamasisha ujenzi wa vituo vya gesi (CNG) na matumizi* 📌 *Aeleza kuhusu kuundwa kwa Timu kuangalia unafuu wa gharama za umeme kwa Wananchi* 📌 *Kapinga azungumzia kazi za kupeleka umeme wa Gridi Rukwa, Kagera, Katavi, Lindi na Mtwara* 📌 *Shilingi Bilioni 9.89 kupeleka umeme jua kwenye visiwa 118* 📌 *Bunge lapitisha Bajeti ya Wizara ya Nishati 2025/2026 kwa asilimia 100* Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt.Doto Biteko amesema dhamira ya Serikali ni kutekeleza mradi mkubwa wa Kuchakata na Kusindika Gesi Asilia (LNG) kutokana na faida zake kiuchumi ila kwa sasa kuna maeneo ambayo Serikali inayafanyia kazi kwa kina kupitia majadiliano na Wawekezaji ili mradi husika uwe na tija kwa nchi na wananchi. Ameyasema hayo tarehe 29 Aprili 2025 bungeni jijini Dodoma wakati akijibu hoja mbalimbali zilizotolewa na Wabunge kuhusu Hotuba ya Ba...

SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA KALI WOTE WANAOTUPA WATOTO.

Image
SERIKALI KUWACHUKULIA HATUA KALI WOTE WANAOTUPA WATOTO. Dodoma Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Mwanaid Ali Khamisi (Mb) amesema Serikali haitasita kuwachukulia hatua kali wale wote ambao wamekuwa wakitupa watoto kwa lengo la kukwepa jukumu lao la msingi la kusimamia malezi, makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto. Mhe. Mwanaii ameyasema hayo Aprili 28, 2025 bungeni Jijini Dodoma wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum (CCM) Fakharia Shomar Khamis aliyetaka kujua kauli ya Serikali juu ya Wanawake wanaotupa watoto. Naibu Waziri Mwanaidi amesema Serikali inakemea na kulaani kitendo cha baadhi ya wanawake kutupa watoto kwa lengo la kukwepa jukumu lao la msingi la kusimamia malezi, makuzi na maendeleo ya awali ya mtoto. "Napenda jamii itambue kuwa Serikali itachukua hatua kali za kisheria dhidi ya wanawake watakaokutwa na hatia ya kutenda kosa hilo na wataadhibiwa kwa mujibu wa Sheria ya Mtoto Sura ya 13, Kanuni ya adhabu Sura ya 16 pamoj...

DC SAME AWASISITIZA WANANCHI KUSHIRIKI KIKAMILIFU KATIKA UCHANGUZI MKUU OCTOBER 2025

Image
 Na Ashrack Miraji kipeo online Media  Mkuu wa Wilaya ya Same, Mhe. Kasilda Mgeni, amewasisitiza wananchi wa wilaya hiyo  kuhakikisha  wanashiriki  kikamilifu katika mchakato wa uchaguzi mkuu wa Rais , wabunge na madiwani Utakao fanyika oktoba mwaka huu, kwa kuchagua viongozi bora watakaobeba shida za wananchi, kutumia haki yao ya kikatiba kugombea nafasi hizo pamoja na kujiepusha na vitendo vya rushwa  ambavyo ni adui wa haki. Mhe. Kasilda ametoa wito huo wakati wa Maadhimisho ya Jubilei ya miaka 50 ya kuzaliwa kwa Dayosisi ya Pare, yaliyofanyika katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Dayosisi ya Pare, Usharika wa Mwembe, kata ya Mwembe, wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro. "Huu ni mwaka wa uchaguzi mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani. Sisi kama kanisa tunayo dhamana kubwa kushiriki kikamilifu katika uchaguzi huu kwa  kuombea uchaguzi huo ili uwe wa amani na utulivu, pamoja na kuhakikisha kwamba sisi waumini tunashiriki kwa kugombea na ku...

DKT.BITEKO AWASILISHA BUNGENI BAJETI YA WIZARA YA NISHATI KWA MWAKA 2025/2026*

Image
📌 *Yagusa utekelezaji wa miradi ya maendeleo kwa asilimia 96.5* 📌 *Upatikanaji umeme wa uhakika. Nishati Safi ya Kupikia, Uendelezaji Gesi Asilia; Baadhi ya vipaumbele vya Bajeti* 📌 *JNHPP, Usambazaji Umeme Vijijini na Ufikishaji Gridi Kigoma; Baadhi ya mafanikio Bajeti 2024/2025* 📌 *Kamati ya Bunge yaridhishwa na utekelezaji wa Bajeti ya Wizara mwaka 2024/2025* Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt.Doto Biteko ameliomba Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuidhinisha Bajeti ya Wizara ya Nishati kwa mwaka 2025/2026 ya kiasi cha shilingi Trilioni 2.2 ambapo asilimia 96.5 ya Bajeti yote ni kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo  na asilimia 3.5 ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida.  Akiwasilisha Bajeti hiyo leo tarehe 28 Aprili, 2025 bungeni jijini Dodoma, Dkt. Biteko ametaja vipaumbele mbalimbali vya Wizara ya Nishati kwa mwaka 2025/2026 ikiwemo kuendelea kuimarisha uzalishaji, usafirishaji na usambazaji wa umeme, pamoja na kufikisha Gridi ya Taifa katika mikoa ili...

UWASILISHWAJI WA BAJETI YA WIZARA YA NISHATI 2025/2026 BUNGENI DODOMA

Image
Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko akiwasilisha Hotuba ya Mapato na Matumizi ya Wizara ya Nishati na Taasisi zake kwa mwaka 2025/2026 bungeni jijini Dodoma. @biteko @wizara_ya_nishati_tanzania @onwm_tanzania @judith__kapinga @bunge.tanzania  

MCHENGERWA: TUULINDE MUUNGANO KWA VIZAZI VYETU

Image
OR-TAMISEMI Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa ametoa wito kwa Watanzania kuuenzi Muungano kwa ajili ya kudumisha amani, umoja na udugu huku akipendekeza kuanzishwa kwa wiki maalum ya Muungano kwa shule zote nchini ili kukuza uelewa wa wanafunzi kuhusu historia ya Muungano. Mhe.Mchengerwa ameyasema hayo katika kijiji cha Sangambi mkoani Mbeya baada ya kukagua na kuweka mawe ya msingi kwenye miradi ya maendeleo yenye thamani ya Sh.bilioni 40 huku wananchi wakimpongeza Mhe.Rais Samia Suluhu Hassan kwa uwekezaji mkubwa. Amehamasisha wasanii na waandishi kuendeleza simulizi za mshikamano wa kitaifa ili kudumisha Muungano huku akiwaasa wazazi kuwaelimisha vijana juu ya thamani ya Muungano. Amesisitiza kuwa Tanzania ni mfano wa amani barani Afrika, tofauti na mataifa mengine yaliyogubikwa na migogoro na kwamba Muungano wa Tanganyika na Zanzibar ulikuwa wa kweli, wa kiitikadi na kimaadili, na umeleta mafanikio makubwa kwa taifa. Waziri Mchengerwa ampongeza Rais ...

MIAKA 61 YA MUUNGANO DKT. BITEKO AHIMIZA VIONGOZI KUACHA ALAMA*

Image
📌 *Asisitiza umoja na ushirikiano Arusha* 📌 *Awataka Watanzania kuenzi Muungano* *Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati* Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amewataka Watanzania kuishi kwa upendo na kushirikiana kwa maslahi mapana ya jamii na Taifa kwa ujumla. Amesema katika kilele cha maadhimisho ya miaka 61 ya Muungano ambapo amewahimiza Watanzania kukumbuka kuwa kuwa Mwl. Julius Nyerere na Hayati Mzee Abeid Amani Karume waliunganisha Tanganyika na Zanzibar katika misingi ya umoja, amani, ushirikiano na kuheshimiana hivyo, muhimu kuendeleza misingi hiyo ili kuenzi Muungano. Dkt. Biteko amesema hayo leo Aprili 26, 2025 katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika Viwanja vya Soko la Kilombero, Wilaya ya Arusha Mjini,  Mkoa wa Arusha. “ Arusha mfanye kazi kwa kushirikiana, muijenge Arusha yenu mkumbuke kwenye nafasi zetu za uongozi mjue kesho hamtakuwepo mtaondoka, kila mahala ulipo acha alama njema itakayo kumbukwa na wengine. Sisi tuliopo ...

MITI 500 YAPANDWA SAME SEKONDARI KUADHIMISHA MIAKA 61 YA MUUNGANO

Image
            Na Ashrack Miraji Kipeo Media Katika kuadhimisha miaka 61 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar, Wilaya ya Same imefanya tukio maalum la upandaji wa miti 500 katika Shule ya Sekondari Same. Tukio hilo limeambatana na wito wa kuendeleza amani, mshikamano, na kulinda mazingira kwa ustawi wa sasa na vizazi vijavyo. Akizungumza kwa niaba ya Mkuu wa Wilaya ya Same, Mhe. Kasilda Mgeni, Katibu Tawala wa Wilaya hiyo, Bi. Upendo Wella, aliwataka wananchi kuuenzi Muungano kwa kudumisha amani, upendo, mshikamano na kutunza mazingira. Alisisitiza kuwa juhudi hizi si tu husaidia maisha yetu ya sasa, bali pia zinaweka msingi bora kwa vizazi vijavyo. Pia, Bi. Wella alieleza kuwa serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, imeweka kipaumbele kikubwa katika masuala ya uhifadhi wa mazingira huku akisisitiza kuwa taasisi za elimu zina jukumu kubwa la kulea kizazi chenye uelewa wa kutosha kuhusu umuhimu wa kuhifadhi mazingira, na akahim...

SERIKALI ITAENDELEA KUBORESHA MIUNDOMBINU YA AFYA – Mhe. KATIMBA

Image
OR-TAMISEMI Naibu Waziri Ofisi ya Rais TAMISEM Mhe. Zainab Katimba amesema Serikali itaendelea kuboresha miundombinu ya afya kwa kutenga bajeti kwa ajili ya ununuzi wa magari ya wagonjwa, vifaa tiba na kuajiri watumishi wa kada mbalimbali za afya kwa ajili ya hospitali za Wilaya nchini ikiwemo Hospitali ya Mabogini.  Mhe. Katimba ameyasema hayo bungeni jijini Dodoma katika kipindi cha Maswali na Majibu, wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti maalumu Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Zuena Athuman Bushiri aliyeuliza. “Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka gari la wagonjwa, vifaa tiba na wataalam katika Hospitali ya Wilaya ya Mabogini, Moshi Vijijini?” “Serikali katika mwaka wa fedha 2021/22 ilinunua magari 594 (ambulance 382 na, usimamizi 212) ya kubebea wagonjwa na usimamizi wa huduma za afya katika Mamlaka za Serikali za Mitaa. Halmashauri ya Wilaya ya Moshi imepokea magari 2 ya kubebea wagonjwa na kupelekwa Kituo cha afya cha Umbwe na Himo.” Amesisitiza Amesema Hospitali ya Wilaya ya M...

MIAKA MINNE YA RAIS SAMIA, ARUMERU YAPOKEA SHILINGI BILIONI 100.6 ZA MAENDELEO

Image
📌 Dkt. Biteko asisitiza Watanzania wasijaribu kuchezea amani 📌 Dkt. Biteko awataka Watanzania kuenzi, kudumisha Muungano  Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema wananchi wa wilayani Arumeru, mkoani Arusha na Watanzania kwa ujumla wana kila sababu ya kumshukuru na kumuombea Rais Mhe. Dkt Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutoa fedha nyingi kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo nchini. Dkt. Biteko amesema hayo leo Aprili 25, 2025 katika mkutano wa hadhara uliofanyika Tengeru Wilaya ya Arumeru, Mkoa wa Arusha ambapo amesema katika kipindi cha miaka minne ya uongozi wa Rais Dkt. Samia wilaya ya Arumeru imepokea zaidi ya shilingi bilioni 100 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maendeleo. “Arusha DC imepata fedha kiasi cha shilingi bilioni 49.6 na Wilaya ya  Arumeru imepokea zaidi ya shilingi  bilioni 51  kwa ajili ya shughuli na miradi mbalimbali ya maendeleo,” amesema Dkt. Bit...

SPIKA BWZ ATAKA WATANZANIA WAUENZI MUUNGANO KWA KUSHIRIKI UCHAGUZI

Image
  Na,AgnesMambo,Tanga . SPIKA wa Baraza la Wawakilishi la Zanzibar Zubeir Ali Maulid, amewataka Watanzania wauenzi na kuulinza Muungano kwa kushiriki uchaguzi Mkuu ujao kwa kuchagua viongozi sahihi. Akizungumza Leo April 25 baada ya kukagua na kuzindua madarasa sita ya shule ya sekondari ya Bushiri wilayani hapa, alisema Muungano ni tunu iliyoasisiwa na viong1ozi hivyo hakuna budi kuulinda kwa nguvu zote. Alisema Watanzania wanapoazimisha miaka 61 ya Muungano, wanatakiwa kukumbuka faida na fursa zilizotokana na Muungano huo lakini pia kutazama namna ya kuepuka chokochoko zenye viashiria vya kuvunja Muungano huo. "Wote hapa zaidi ya asilimia 80 tuliopo hapa tumezaliwa ndani ya Muungano hivyo tunayo sababu kubwa ya kuenzi, kuulinda kwa kushiriki uchaguzi Mkuu ujao ili tuwapate viongozi wetu," alisema na kuongeza, "Tunapoadhimisha maadhimisho ya miaka 61 ya Muungano wetu tunatakiwa tukumbuke faida na fursa zilizopatikana kupitia Muungano wetu,". Akizungumza kuhusu shul...

RC BATLIDA ATAKA UKARABATI SOKO LA NGAMIANI UHAKIRISHWE KABLA YA MVUA KUBWA

Image
  Na,Agnes Mambo kipeo online Media  MKUU wa mkoa wa Tanga, Balozi Dkt Batlida Burian ameiagiza halmashauri ya Jiji la Tanga, kuharakisha ukarabati wa soko la Ngamiani ili mvua zinazoendelea kunyesha zisiharibu bidhaa za wafanyabiashara. Akizungumza katika soko hilo April 25/2025 majira ya saa Moja kamili Asubuhi alipofika kukagua na kuona shughuli za wafanyabiashara hao, Dkt Batlida aliagiza mkandarasi anayekarabati soko hilo awe na wafanyakazi wa kutosha ili kazi hiyo isichukue muda mrefu. "Mkurugenzi hakikisheni kazi ya ukarabati inakwenda kwa haraka, mnajua kipindi hiki ni cha mvua lazima tulinde bidhaa za wafanyabiashara wetu, hakikisheni mnakuwa na wafanyakazi wa kutosha ikibidi tunaweza kuongeza wafungwa ili soko likamilike kwa haraka," alisema Mkuu wa mkoa. Mkuu wa mkoa aliwataka wafanyabiashara wawe watulivu katika kipindi hiki cha matengenezo na kwakuwa soko linakarabatiwa huku wakiendelea kuuza bidhaa zao basi wasiwe kikwazo kwa wafanyakazi wa mkandarasi. Alimwagiz...

SERIKALI KUENDELEA KUWEKEZA KATIKA SEKTA YA AFYA - DKT. BITEKO

Image
📌 Dkt. Biteko atambelea Hospitali ya Wilaya ya Meru Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Serikali imeahidi kuendelea kuboresha huduma za Afya nchini katika ngazi zote ili kuboresha huduma za Afya kwa Watanzania. Hayo yamesemwa Aprili, 25, 2025 na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko akiwa ziarani Mkoani Arusha ambapo amesema kuwa lengo la uwekezaji katika sekta ya afya ni kusigeza huduma za afya kwa wananchi." Serikali inayoongozwa na Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea na uwekezaji mkubwa unaofanya kwa kujenga hospitali, vituo vya afya na zahanati katika maeneo mbalimbali nchini. Akizungumza baada kutembelea Hospitali ya Wilaya ya Meru, iliyopo Wilaya ya Arumeru, Mkoa wa Arusha, Mhe. Dkt. Biteko amesema lengo la uwekezaji katika sekta ya afya ni kuboresha afya za Watanzania. “ Kama mnavyofahamu afya ndio mtaji wa wananchi na Serikali itaendelea kuboresha huduma za afya kwa kujenga hospitali mpya na kufanyia ukarabati zilizopo,” a...