Posts

Showing posts from March, 2025

WANANCHI KILIMANJARO WAISHUKURU SERIKALI KUPELEKA MADAKTARI BINGWA WA MACHO.

Image
  WALIOSUMBULIWA NA MACHO KILIMANJARO WAISHUKURU SERIKALI KUPELEKA MADAKTARI BINGWA WA MACHO. Na Mwandishi Wetu.  Same, Kilimanjaro. Wananchi waliokuwa wakikabiliwa na matatizo ya kuona mkoani Kilimanjaro wameishukuru Serikali kwa kuwaletea madaktari bingwa wa macho kutoka nchini Marekani na kuwafanyia uchunguzi wa magonjwa hayo na ushauri wa kitaalam, tiba kwa upasuaji wa mtoto wa jicho na kuweza kuona upya. Madaktari hao ambao wamepiga kambi ya wiki mbili katika hospitali ya Wilaya ya Same ambapo watu zaidi ya elfu mbili (2000) wamefanyiwa uchunguzi huku wagonjwa zaidi ya tisini (90) wamefanyiwa upasuaji wa mtoto wa jicho. Wakizungumza kwa nyakati tofauti hospitalini hapo mmoja kati ya wagonjwa waliofanyiwa upasuaji wa mtoto wa jicho Bw. Idd Mlaki, Mkazi wa Kileo wilayani Mwanga alieleza kuwa kwa muda wa miezi sita alikuwa haoni tatizo ambalo lilianza ghafla ambapo kwa sasa mara baada ya kupata huduma hiyo hali yake ya kuona imerejea tena. “Macho yangu yalikufa ghafl...

WAZIRI ULEGA AWASIMAMISHA KAZI WATUMISHI WA MIZANI KUPISHA UCHUNGUZI

Image
WAZIRI ULEGA AWASIMAMISHA KAZI WATUMISHI WA MIZANI KUPISHA UCHUNGUZI. Na Mwandishi Wetu.  Dodoma.  Waziri wa Wizara ya Ujenzi, Abdallah Ulega amemuelekeza Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi Mhandisi Balozi Aisha Amour, kuwasimamisha kazi wasimamizi wote wa Mizani waliokuwa zamu katika Mizani zilizopo katika barabara kuu ya T1 inayoanzia Dar es Salaam – Zambia kupitia mpaka wa Tunduma kwa ajili ya kupisha uchunguzi wa malalamiko katika Mizani hizo. Ulega amefanya maamuzi hayo mara baada ya kadhia iliyojitokeza hivi karibuni kwa msafirishaji Bi. Pamela James Bukumbi mwenye gari ya mizigo namba T 137 DLQ likiwa na tela T 567 CUR iliyotokea katika kituo cha Mizani ya Vigwaza akilalamika kuhusu kutozwa faini ya kuzidisha uzito katika Mizani hiyo wakati mizani nyingine alizopita gari yake haikuwa imezidisha uzito.  Ulega ametoa maelekezo hayo jijini Dodoma leo tarehe 20 Machi, 2025 mara baada ya kupata taarifa hiyo na kusikiliza pande zote mbili kutoka kwa mlalamikaji na mlalamiki...

WATAKAOBAINIKA KUHUSIKA KUCHOMA MOTO BWENI LA WANAFUNZI SHULE YA SEKONDARI MAKANYA KUCHUKULIWA HATUA.

Image
WATAKAOBAINIKA KUHUSIKA KUCHOMA MOTO BWENI LA WANAFUNZI SHULE YA SEKONDARI MAKANYA KUCHUKULIWA HATUA.  Na Christina Thomas.  Same, Kilimanjaro.  Mkuu wa Wilaya ya Same, Mhe. Kasilda Mgeni, amesema kuwa serikali haitasita kuchukua hatua kali za kinidhamu, ikiwemo kuwafukuza shule wale wote watakaobainika kuhusika na tukio la moto lililoteketeza jengo la bweni la wanafunzi wa kike katika Shule ya Sekondari Makanya. Moto huo ulisababisha uharibifu mkubwa wa miundombinu, kuteketeza vifaa vya wanafunzi kama magodoro, nguo, madaftari na mali nyinginezo. Akizungumza wakati wa kupokea msaada wa vifaa mbalimbali kutoka kwa wadau wa maendeleo wilayani Same, Mhe. Kasilda Mgeni alieleza kuwa uchunguzi wa tukio hilo uko katika hatua za mwisho na kuahidi kuwa wahusika wote watachukuliwa hatua kwa mujibu wa sheria. "Hili jambo lilinisikitisha sana. Yeyote atakayebainika, iwe ni mwalimu au mwanafunzi, atachukuliwa hatua za kinidhamu, ikiwa ni pamoja na kufukuzwa shule. Tukio hili ni baya...

KAMATI YA BUNGE YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO KATIKA HIFADHI YA MAKUYUNI

Image
KAMATI YA BUNGE YARIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO KATIKA HIFADHI YA MAKUYUNI Na. Mwandishi Wetu.  Arusha. Kamati ya kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii yaridhishwa na utekelezaji wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa na Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA), katika Hifadhi ya Wanyamapori Makuyuni almaarufu kama "Makuyuni Wildlife Park" iliyopo Wilaya ya Monduli, Mkoani Arusha. Akizungumza baada ya kutembelea hifadhi hiyo, tarehe 13 Machi, 2025, Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Ardhi, Maliasili na Utalii, Mhe. Timotheo Mnzava (Mb) alisema Kamati imeridhishwa na utekelezaji wa miradi hiyo ambayo ni ujenzi wa barabara yenye urefu wa kilometa 30 iliyogharimu shillingi milioni 256 pamoja na bwawa lenye uwezo wa kubeba maji lita milioni 52 lililogharimu shilingi milioni 125. "Kwanza tuipongeze Serikali kwa hatua ya kuchukua eneo hili muhimu na kuwakabidhi TAWA, pia niwapongeze TAWA kwa ukarabati na ufunguaji wa barabara wa hi...

WITO WATOLEWA KUWACHUKULIA HATUA ZA KIUTUMISHI MAAFISA UTUMISHI WAZEMBE WANAOWAKOSESHA HAKI ZA MSINGI WALIMU.

Image
WITO WATOLEWA KUWACHUKULIA HATUA ZA KIUTUMISHI MAAFISA UTUMISHI WAZEMBE WANAOWAKOSESHA HAKI ZA MSINGI WALIMU. Na Christina Thomas Same, Kilimanjaro.  Imeelezwa kuwa Watumishi wa kada ya Ualimu  wakabiliwa na changamoto mbalimbali ikiwemo kucheleweshwa kupandishwa madaraja, kubadilishwa kwa miundo baada ya kujiendeleza, malimbikizo ya mishahara, madai ya muda mrefu ya stahiki za uhamisho, taarifa chafu kwenye mfumo pamoja na madai ya kustaafu ambapo baadhi ya changamoto hizo zimetajwa kusababishwa na baadhi ya maafisa utumishi wazembe wanaowakosesha haki za msingi watumishi wa Umma wakiwemo walimu. Kutokana na hilo, Mkuu wa Wilaya ya Same, Mhe. Kasilda Mgeni, amesisitiza kuwa ni vyema mamlaka husika kuwachukulia hatua baadhi ya maafisa Utumishi ambao watabainika kufanya uzembe kwa makusudi kuwakosesha haki za msingi watumishi wa Umma wakiwemo walimu ili iwe fundisho kwa wengine wenye tabia kama hizo. Akizungumza katika kliniki ya kutatua changamoto za walimu (Samia Teacher's Mo...

RAIS SAMIA AZINDUA MRADI WA MAJI WA SAME-MWANGA-KOROGWE.

Image
RAIS SAMIA AZINDUA MRADI WA MAJI WA SAME-MWANGA-KOROGWE. Mwanga, Machi 9, 2025 Na Musa Mathias.  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo amezindua rasmi Mradi wa Maji wa Same-Mwanga-Korogwe katika hafla iliyofanyika wilayani Mwanga, mkoani Kilimanjaro. Mradi huu mkubwa, ambao umekuwa ukisuasua kwa takriban miaka 20, sasa umekamilika na utawezesha upatikanaji wa maji safi na salama kwa wakazi wa wilaya za Same, Mwanga, na Korogwe. Katika hotuba yake, Rais Samia mara baada ya kuzindua mradi wa maji Same-Mwanga-Korogwe, akiwa katika mkutano wa hadhara na wananchi wa mkoa wa Kilimanjaro alielezea changamoto zilizokumba utekelezaji wa mradi huu, ikiwemo kusukumana, kusutana, na hata kushitakiana na makandarasi.  “Leo tunashuhudia matunda ya uvumilivu na juhudi za pamoja. Mradi huu ulianza kwa ahadi tangu enzi za watanyulizibwangu, lakini sasa, miaka kadhaa baadaye, tumeweza kuutekeleza na wananchi wameanza kunufaika,” alisema Rais Samia. Ra...

JUHUDI ZA RAIS SAMIA, NEEMA KWA WANANCHI KUPITIA MRADI WA MAJI SAME-MWANGA-KOROGWE

Image
JUHUDI ZA RAIS SAMIA, NEEMA KWA WANANCHI KUPITIA MRADI WA MAJI SAME-MWANGA-KOROGWE Na Mwandishi Wetu.  Kilimanjaro.  Mkuu wa Wilaya ya Same, Mhe. Kasilda Mgeni akiongozana na wajumbe wa kamati ya Ulinzi na Usalama ya Wilaya hiyo, leo machi 03, 2025 wametembelea mradi mkubwa wa maji wa Same-Mwanga-Korogwe, Ziara hii imelenga kukagua maendeleo ya mradi huo unaotekelezwa kwa lengo la kuboresha upatikanaji wa maji safi na salama kwa wakazi wa mikoa ya Kilimanjaro na Tanga. Katika ziara hiyo, Meneja wa Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Same-Mwanga (SAMWASA), Mhandisi Rashidi Mwinjuma, alieleza kuwa mradi huu umefikia hatua nzuri ya utekelezaji na unatarajiwa kuongeza upatikanaji wa maji safi kwa wananchi wa Same, Mwanga na Korogwe. Mradi wa maji wa Same-Mwanga-Korogwe unalenga kuhudumia zaidi ya wakazi milioni moja, ikiwa ni hatua muhimu katika kuimarisha huduma za maji safi na usafi wa mazingira. Kupitia mradi huu, changamoto za upatikanaji wa maji katika maeneo husika zi...