Posts

Showing posts from September, 2025

KURA ZOTE BUTINZYA TUMPIGIE DKT. SAMIA - DKT. BITEKO

Image
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Bukombe kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Doto Mashaka Biteko amewahimiza wananchi wa Kata ya Butinzya, Wilayani Bukombe kumpigia kura mgombea wa Urais kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM)Dkt. Samia Suluhu Hassan ili aendelee kuongoza na kusimamia miradi ya maendele iliyokwishaanzishwa na hivyo kuwaletea maendeleo. Dkt. Biteko amesema hayo Septemba 30, 2025 wakati wa mkutano wa kampeni katika Kata ya Butinzya wilayani Bukombe mkoani Geita ikiwa ni sehemu Kampeni za Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani utakaofanyika Oktoba 29, mwaka huu. Amesema wananchi wanalo jukumu la kujotokeza kwa wingi kupiga kura na watakapopiga kura maana yake ni kutimiza wajibu wao kidemokrasia ambao utawawezesha kutimiziwa mahitaji yao kwa kujengewa miradi ya maji, umeme, barabara, hospitali na shule. Amesema katika miaka mitano iliyopita wananchi hao wakishiriki katika kutekeleza miradi ya maendeleo iliyolenga kutatua changamoto za Bukombe na sasa jukumu lililo...

NGORONGORO YAENDELEA NA KUBORESHA HUDUMA YA MAJI SAFI NA MIUNDOMBINU KWA AJILI YA WANANCHI

Image
Mamlaka ya Hifadhi ya eneo la Ngorongoro kupitia Idara ya Maendeleo ya Jamii  imetembelea kijiji cha Olpiro kilichopo Kata ya Eyasi, wilayani Ngorongoro, na kuchukua hatua za kutatua changamoto ya upatikanaji wa maji safi na salama kwa wananchi pamoja na mifugo yao. Wataalam kutoka NCAA katika ziara iliyofanyika  Septemba 30, 2025, wamekagua marekebisho na ukarabati wa miundombinu ya maji uliofanyika katika kijiji hicho, hatua iliyowawezesha wananchi kupata huduma ya maji safi na salama. Ukarabati wa miundombinu  ya huduma ya maji katika kijiji hicho umeleta faraja kubwa kwa wananchi hao waliokuwa wakikabiliwa na changamoto ya uhaba wa maji kwa muda mrefu. Aidha, pamoja na maboresho ya huduma ya maji, NCAA pia imefanya tathmini ya miundombinu mingine ikiwemo josho la kuogeshea mifugo lililopo katika kijiji hicho. Wananchi wa kijiji cha Olpiro wameipongeza Serikali kupitia mamlaka ya hifadhi ya Ngorongoro kwa jitihada hizo wakieleza kuwa zinachangia sio tu katika kuboresha...

DKT BITEKO AWAPA HEKO WACHIMBAJI WADOGO WA MADINI

Image
📌 *Mchango wa wachimbaji wadogo wa madini waongezeka kutoka 20% mwaka 2020 hadi 40% mwaka 2024* 📌 *Teknolojia za kisasa za uchenjuaji madini zatajwa kuwa na tija kuliko matumizi ya zebaki* 📌 *Serikali kuendelea kuweka mazingira wezeshi kwa ajili ya maendeleo ya sekta ya madini* 📌 *Mwaka 2020/2021 hadi 2024/2025 Serikali yakusanya zaidi ya shilingi tirioni 3.8 kutoka sekta ya madini* *Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati* Serikali imeongeza ushirikishwaji wa Watanzania katika Sekta ya Madini ikiwa ni pamoja na shughuli zote za mnyororo mzima wa thamani wa madini nchini ambapo kwa Mkoa wa Geita pekee wachimbaji wadogo wamezalisha kilo 22,014.61 zenye thamani ya shilingi trilioni 3.443 na Serikali kukusanya mapato ya shilingi bilioni 2.5 katika kipindi cha mwaka 2021/2022 hadi 2024/2025. Mchango wa wachimbaji wadogo wa madini umeongezeka kutoka asilimia 20 mwaka 2020 hadi kufikia asilimia 40 mwaka 2024 katika mapato yote ya sekta ya madini na mchango wa Sekta ya Madini k...

TARURA KUPITIA DARAJA LA MAWE MAJIMOTO KUKUZA SEKTA YA KILIMO, MPIMBWE-KATAVI*

Image
📌Mradi wote wafikia  95% ya utekelezaji  Mpimbwe, Katavi Ujenzi wa Daraja la mawe katika mto Katupa sambamba na ujenzi wa barabara ya Majimoto-Namanyele inayojengwa kiwango cha changarawe katika Halmashauri ya Mpimbwe Mkoani Katavi umetajwa kukuza sekta ya kilimo na kuboresha uchumi wa Wakulima. Meneja wa Wakala ya Barabara Vijijini na Mijini (TARURA) Wilaya ya Mlele Mhandisi Paul Mabaya, amesema thamani ya ujenzi wa mradi huo ni shilingi 361,950,000.00 ambapo utekelezaji wake umefikia asilimia 95.  Mhandisi Mabaya amesema mradi huo pia unajumuisha ujenzi wa Daraja la mawe, barabara ya kiwango cha changarawe kilomita 1.5 na ujenzi wa kalvati tatu huku fedha za utekelezaji wa mradi huo ni sehemu za fedha za ufadhili kutoka Benki ya Dunia kupitia mradi wa  "RISE"  Kwa upande wake, Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa  mwaka 2025 Ndugu Ismail Ali Ussi amesema dhamira ya serikali ni kuhakikisha wananchi wake wanakuwa na miundombinu wezeshi kwa ajili ya ...

UN YAITAJA TANZANIA KINARA ONGEZEKO LA WATALII

Image
Na Mwandishi Wetu TANZANIA imejumuika na mataifa mengine duniani kuadhimisha Siku ya Utalii Duniani inayofanyika Septemba 27 kila mwaka, huku imeendelea kutajwa na Shirika la Utalii Duniani kuwa miongoni mwa nchi zinazoongoza Afrika kwa ongezeko kubwa la idadi ya watalii. Akizungumza  kwenye kilele cha maadhimisho hayo yaliyofanyika katika eneo la Hifadhi ya Ngorongoro (picnic site), Katibu Mkuu wa Wizara ya Maliasili na Utalii, Dkt. Hassan Abbasi amesema ripoti ya UN Tourism ya mwaka 2024 imeitaja Tanzania kuwa kinara barani Afrika katika ongezeko la watalii baada ya janga la UVIKO-19, kwa ukuaji wa asilimia 48, ikifuatiwa na Ethiopia (40%), Morocco (35%), Kenya (11%) na Tunisia (9%). Dkt. Abbasi amesema ripoti ya mwaka huu (2025) imeionyesha Tanzania kuwa miongoni mwa nchi 20 bora duniani zinazofanya vizuri katika sekta ya utalii, kwa wastani wa ukuaji zaidi ya asilimia 50. "Idadi ya watalii wa kimataifa iliongezeka kutoka 922,692 mwaka 2021 hadi kufikia 2,141,895 mwaka 2024, sa...

KASIKI AWAPIGA MSASA WADAU WA SEKTA YA MADINI*

Image
- *Abainisha fursa kubwa zilizopo kwenye mnyororo wa thamani* *Ajira zaongezeka mara tatu tangu 2018* MKURUGENZI wa Ukaguzi na Biashara ya Madini katika Tume ya Madini (MATD), CPA. Venance Kasiki, amewataka wadau wa Sekta ya Madini kuongeza ubunifu na ushiriki endelevu kwenye shughuli za uchumi wa madini kwa kuanzisha viwanda vya kuzalisha bidhaa zinazohitajika migodini badala ya kuendelea kuwa mawakala wa wazalishaji wa kigeni (OEMs). Akizungumza  katika Maonesho ya Nane ya Kitaifa ya Teknolojia ya Madini yanayoendelea mjini Geita, Kasiki alisema ushiriki wenye tija unahitaji kampuni kuwa na mifumo madhubuti ya uendeshaji na usimamizi, kutoa bidhaa na huduma bora kwa wakati, kujifunza teknolojia mpya, pamoja na kushirikiana katika kuunda mitaji mikubwa ya pamoja. Alibainisha kuwa mnyororo wa thamani wa madini una fursa nyingi zinazoweza kushughulikiwa na Watanzania ikiwemo usambazaji wa mitambo ya migodini, huduma za TEHAMA, usafirishaji, fedha na bima, huduma za vyakula, vifaa ki...

KILA JIWE LINA THAMANI – KERAKA

Image
Geita MJIOLOJIA kutoka Ofisi ya  Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Mara, Godfrey Keraka, amesema kuwa kila jiwe lina thamani kwa sababu ya mchango wake katika sekta ya madini, maendeleo ya taifa na teknolojia ya kisasa duniani. Akizungumza kwenye Maonesho ya Kimataifa ya Teknolojia ya Madini yanayoendelea mkoani Geita, Keraka ameeleza kuwa sekta ya madini inachangia  asilimia 10.1 ya Pato la Taifa (GDP) na ni urithi muhimu wa nchi unaopaswa kulindwa. Ametolea mfano wa madini ya vito kama Amethyst, Rose-Quartz na Quartz ambayo hutumika kutengeneza mapambo ya thamani, wakati madini ya chuma yanahusishwa zaidi na ujenzi wa miundombinu, utengenezaji wa magari, meli na mashine mbalimbali. Aidha, shaba hutumika kwenye nyaya za umeme, feldspar kwenye vigae na mapambo, na pyrite kwenye mbolea, mapambo pamoja na uzalishaji wa tindikali ya salfyuriki. Kwa upande mwingine, makaa ya mawe yametajwa kuwa chanzo muhimu cha nishati, huku dhahabu na fedha zikibainishwa kama madini yenye thamani ku...

UTENDAJI KAZI WA WIZARA YA NISHATI NA TAASISI ZAKE WAIMARIKA

Image
📌 *Wapanda kutoka asilimia 95 hadi 96.16 katika kipindi cha robo mwaka* 📌 *Mhandisi Mramba asema ongezeko hilo linaakisi utoaji wa huduma kwa wananchi* 📌 *Apongeza Taasisi kuendelea kuboresha utoaji huduma kwa Wananchi.* 📌 *Asisitiza mitandao ya kijamii kutumika ipasavyo utoaji elimu Nishati Safi ya kupikia.* Imeelezwa kuwa, utendaji kazi wa Wizara ya Nishati kupitia Taasisi inazosisimamia umezidi kuimarika na kufikia asilimia 96.16 katika kipindi cha robo nne ya mwaka 2024/2025. Hayo yamefahamika wakati wa kikao cha Tano cha Tathmini ya utendaji kazi wa Wizara ya Nishati  na Taasisi zake kwa robo nne ya mwaka 2024/2025 kilichofanyika jijini Dodoma  na kuongozwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati Mhandisi Felchesmi Mramba. Tathmini hiyo ya utendaji kazi iliyofanywa na Kitengo cha Ufuatiliaji na Tathmini katika Wizara ya Nishati imeonesha kuwa katika kipindi cha robo ya nne ya mwaka 2024/2025 utendaji kazi wa Taasisi zilizochini ya Wizara ya Nishati  umeimarika kwa za...

MWANZA PRECIOUS METALS REFINERY YAKUSANYA ZAIDI YA TANI 5 ZA DHAHABU KWA NIABA YA BOT

Image
📍Mwanza Kiwanda cha kusafisha madini ya dhahabu cha Mwanza Precious Metals Refinery (MPMR) kilichopo jijini Mwanza, kimefanikiwa kukusanya zaidi ya tani tano za dhahabu kwa niaba ya Benki Kuu ya Tanzania (BOT). Hayo yamesemwa na Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Mwanza, Mhandisi Nyaisara Mgaya, alipokuwa akizungumza na ujumbe kutoka nchini Malawi uliotembelea mkoani humo kwa lengo la kujifunza kuhusu usimamizi na uendeshaji wa biashara ya madini, hususan mfumo wa masoko unaotumika nchini Tanzania. Mhandisi Mgaya amesema kuwa kiwanda hicho kina uwezo wa kusafisha hadi kilo 960 za dhahabu kwa siku, ingawa kwa sasa kinatumia mashine zenye uwezo wa kusafisha kilo 480 kwa siku, kutokana na upatikanaji wa malighafi. Katika kikao hicho, kiongozi wa ujumbe kutoka Malawi, ambaye pia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Maendeleo ya Biashara za Vikundi nchini humo, Zizwan Khonje, amemshukuru Afisa Madini wa Mkoa wa Mwanza kwa elimu waliyoipata kuhusu mfumo wa biashara na masoko ya madini hapa nchini. “Tanzani...

DKT. BITEKO AMPA POLE RAIS MWINYI, ASHIRIKI MAZISHI YA KAKA YAKE

Image
Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko ameungana na mamia ya waombolezaji kutoa pole kwa familia ya Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi kufuatia kifo cha kaka yake Abass Mwinyi ambaye pia alikuwa mgombea Ubunge wa Jimbo la Fuoni kilichotokea Zanzibar, Unguja  usiku wa kuamkia Septemba 25, 2025. Dkt. Biteko ameshiriki mazishi hayo Septemba 26, 2025 Bumbubwini Mangapwani, Zanzibar. Ambapo ameungana na viongozi mbalimbali akiwemo Mgombea Mwenza wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi, Makamu Mwenyekiti wa CCM Taifa, Ndugu Stephen Wasira, Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa, Makamu wa pili wa Rais wa Zanzibar, Mhe. Hemed Suleiman Abdulla . Aidha, baada ya mazishi baadhi viongozi walipata fursa ya kutoa heshima katika kaburi la Hayati Ali Hassan mwinyi lililopo Bumbubwini Mangapwani, Zanzibar. Awali, Rais wa Jamhuri ya Muungano w...

RAS NZOWA: KAMILISHENI MIRADI KWA WAKATI

Image
RAS NZOWA: KAMILISHENI MIRADI KWA WAKATI Na Musa Mathias. Same - Kilimanjaro. Katibu Tawala wa Mkoa wa Kilimanjaro, Bw. Kiseo Nzowa, ameielekeza Halmashauri ya Wilaya ya Same kuhakikisha inakamilisha kwa wakati miradi ya maendeleo inayotekelezwa kwa fedha za Serikali ya Awamu ya Sita, ili wananchi waanze kunufaika mapema na huduma bora. Bw. Nzowa ametoa maagizo hayo, wakati wa ziara yake ya kikazi wilayani Same, alipoambatana na Sekretarieti ya Mkoa na kukagua miradi mitatu ya maendeleo sekta ya elimu yenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni 1.1. Alisisitiza kuwa dhamira ya serikali ni kuona kila mradi unakamilika kwa muda uliopangwa, kwa viwango bora, na kuanza kutoa huduma kwa wananchi bila ucheleweshaji. Miradi iliyokaguliwa ni pamoja na ujenzi wa shule mpya ya sekondari ya Amali, Kata ya Kihurio, unaogharimu zaidi ya shilingi milioni 584 na unatarajiwa kuanza kutumika Januari 2026 kwa kudahiri wanafunzi 80 katika mikondo miwili. Mradi mwingine ni ujenzi wa bwalo la chakula la wan...