Posts

Showing posts from September, 2025

WAFANYABIASHARA WAONGEZE USAHIHI: RISITI KILA UNUNUZI

Image
WAFANYABIASHARA WAONGEZE USAHIHI: RISITI KILA UNUNUZI Subscribe Channel yetu ya Youtube hapa youtube.com/@kipeoonlinemedia?si=vZ45foO1hBmK1xvX  Na Musa Mathias Kipeo Online Media  Mkuu wa Wilaya ya Same, Kasilda Mgeni, amewataka wafanyabiashara kuendelea kutumia mashine za kielektroniki za kodi (EFD) na kuhakikisha kila mteja anapata risiti halali. Lengo kuu ni kupunguza mianya ya upotevu wa mapato ya serikali. Akizungumza katika kikao cha Kamati ya Ushauri wa Kodi cha Wilaya,  Kasilda alisisitiza kuwa ni jukumu la kila mfanyabiashara kutoa risiti kwa kila mauzo anayofanya, huku akiwaasa wateja kudai risiti wanaponunua bidhaa. “Tunatakiwa kuendelea kuwaelimisha wafanyabiashara kutumia mashine za EFD, kutoa risiti kwa wateja huku wateja wakisisitizwa kudai risiti wanaponunua bidhaa, ili kulinda mapato ya serikali yasipotee,” alisema Kasilda. ​Kwa upande wake, Meneja wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Wilaya ya Same, Eliapenda Mwanri, alieleza kuwa taasisi hiyo imefanikiwa...

DC KASILDA APONGEZA UJENZI WA SOVAVI SEKONDARI: “NI UWEKEZAJI KWA TAIFA”

Image
Na Ashrack Miraji Ujenzi wa Shule mpya ya Sekondari Sovavi iliyopo Kata ya Hedaru, wilayani Same, umefikia asilimia 85 na unatarajiwa kukamilika ifikapo Septemba 30, 2025. Mradi huo unatajwa kuwa suluhisho muhimu kwa changamoto zinazowakabili wanafunzi wa eneo hilo, ikiwemo kutembea umbali mrefu kwenda shule na msongamano mkubwa katika Shule ya Sekondari Mkombozi. Hayo yamebainika wakati wa ziara ya Mkuu wa Wilaya ya Same, Mhe. Kasilda Mgeni, aliyeongozana na Kamati ya Usalama ya Wilaya kukagua maendeleo ya ujenzi huo. Mhe. Kasilda amepongeza hatua iliyofikiwa na kutoa wito kwa mafundi pamoja na Kamati ya Ujenzi kuhakikisha mradi unakamilika kwa wakati na kwa ubora unaotakiwa. “Ujenzi wa shule hii ni kielelezo cha jitihada za serikali katika kuwekeza kwenye sekta ya elimu, jambo linaloendana na azma ya kitaifa ya kuinua viwango vya ufaulu na kukuza rasilimali watu wa taifa. Tutaendelea kuimarisha miundombinu ya elimu ili wanafunzi waweze kunufaika kwa ubora,” alisema Mhe. Kasilda. Aidh...

WIZARA YA MAENDELEO YA JAMII JINSIA WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM INAWATAKIA HERI YA SIKUKUU YA MAULID

Image

TANESCO INAWATAKIA HERI YA SIKUKUU YA MAULID

Image
 

DKT JINGU AZINDUA KAMATI YA MAKAO YA TAIFA YA WATOTO KIKOMBO.

Image
Na WMJJWM-Dodoma. Serikali inaendelea kuweka mazingira mazuri na rafiki kwa ajili ya ustawi wa watoto nchini kupitia utekelezaji na uimarishaji wa afua mbalimbali hususan watoto waliotokea katika mazingira magumu. Hayo yamebainishwa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Dkt. John Jingu katika uzinduzi wa Kamati ya makao ya Taifa ya Watoto Kikombo Septemba 04, 2025 Katika ukumbi wa Wizara jijini Dodoma. Dkt. Jingu ameeleza kwamba uwepo wa Kamati hiyo ni moja ya uimarishaji wa afua ya kuboresha ustawi wa watoto hasa waliotokea katika mazingira magumu ili kuhakikisha wanapata malezi na makuzi stahiki kama yale yanayopatikana watoto waliopo kwenye familia ili waweze kufikia utimilifu wao kupata taifa bora. “Sote tunafahamu kuwa sehemu sahihi na muhimu ya kumlelea mtoto ni kwenye familia lakini sababu ya changamoto mbalimbali baadhi ya watoto hujikuta kulelewa kwenye familia imeshindikana na hapo ndipo nguvu ya taifa inaingia ili kuhakikisha ...

WIZARA YA NISHATI INAWATAKIA HERI YA SIKUKUU YA MAULID

Image
 Katika kipindi hiki cha Maulid, Wizara ya Nishati inawatakia wananchi wote maadhimisho mema yenye amani, mshikamano na matumaini. #Maulid Njema #NishatiTupoKazini

UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI SOVAVI WAFIKIA ASILIMIA 85, UNATARAJIWA KUKAMILIKA SEPTEMBA 30

Image
UJENZI WA SHULE YA SEKONDARI SOVAVI WAFIKIA ASILIMIA 85. Na Christina Thomas. Same, Kilimanjaro.  Tafadhali subscribe Youtube Channel yetu hapa Ujenzi wa mradi wa shule mpya ya Sekondari ya Kata ya Hedaru (Sovavi Sekondari) iliyopo wilayani Same umefikia asilimia 85 ambao unatarajiwa kukamilika ifikapo Septemba 30, 2025, jambo linalotajwa kuwa suluhisho kubwa kwa changamoto zinazowakabili wanafunzi wa eneo hilo ikiwemo kutembea umbali mrefu kwenda shule na msongamano katika Shule ya Sekondari Mkombozi. Hayo yamebainishwa wakati wa ziara ya Mkuu wa Wilaya ya Same, Mhe. Kasilda Mgeni, Septemba 3, 2025, alipotembelea na kukagua maendeleo ya mradi huo akiambatana na Kamati ya Usalama ya Wilaya. Mkuu wa Wilaya ya Same, Bi. Kasilda Mgeni akikagua moja ya dirisha katika majengo ya shule mpya ya sekondari ya kata ya Hedaru (Sovavi sekondari). Picha na Musa Mathias. Mhe. Mgeni amewataka mafundi na Kamati ya Ujenzi kuhakikisha mradi huo unakamilika kwa wakati uliopangwa, akisisitiza kuwa ser...

TANESCO YAFANYA MATENGENEZO KINGA BILA KUZIMA UMEME NJIA YA KUSAFIRISHA UMEME CHALINZE - KINYEREZI*

Image
📍*Ni kwa kutumia teknolojia ya Live Line 📍*Wananchi waendelea kufurahia huduma ya umeme huku matengenezo yakiendelea* Na Charles Kombe, Chalinze Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limefanya matengenezo kinga kwenye njia ya kusafirisha umeme wa msongo wa Kilovoti 220 kutoka Kituo cha kupoza umeme cha Chalinze hadi Kituo cha Kinyerezi Dar es Salaam bila kuzima umeme (live line). Matengenezo hayo yalihusisha ubadilishaji wa vikombe (insulator) ambavyo vilionekana kuwa na changamoto katika ukaguzi uliofanywa kwenye njia hiyo ya kusafirisha umeme ambapo hapo awali ingelazimu kuzima umeme kwenye laini hiyo ambapo ingepelekea maeneo yanayopata umeme kupitia njia hiyo kukosa huduma kipindi cha matengenezo .  Akingunzumza wakati wa zoezi hilo Mhandisi kutoka Kitengo cha usafirishaji umeme Philemon Tirukaizile alisema teknolojia hiyo  imeondoa kero ya kukatika umeme kwa wananchi wakati wa matengenezo.  “Bila kuwa  na teknolojia hii  ya  kufanya matengenezo bila...

TANESCO KUWAFIKISHA KWENYE VYOMBO VYA SHERIA WANAOHUJUMU MIUNDOMBINU YA UMEME KARIAKOO

Image
Katika kuhakikisha vitendo vya wizi na uharibifu wa  miundombinu ya umeme vinakomeshwa nchini, TANESCO  itawafikisha katika vyombo vya sheria baadhi ya wafanyabiashara waliobainika kutumia umeme kinyume na  utaratibu baada ya kuchepusha baadhi ya Nyaya kwenye mita ili kuzifanya mita hizo kushindwa kuhesabu umeme unaotumika. Akizungumza Septemba 03,2025  katika operesheni ya kuwasaka wahujumu wa miundombinu ya umeme katika eneo la Kariakoo mtaa wa Agrey Mhandisi Mohamed Lacha wa  kitengo cha kudhibiti mapato TANESCO alieleza kuwa  matukio kama hayo yanaikosesha  Shirika mapato hivyo  waliohusika na matukio hayo  watafikishwa kwenye vyombo vya sheria  na kusitishiwa huduma ya umeme na kutakiwa kulipa deni wanalodaiwa. ‘’Watu hawa wanatarajiwa kuchukuliwa hatua za kisheria lakini pia sisi kama TANESCO tutawasitishia huduma ya umeme na  watalazimika kulipa deni lote wanalodaiwa kwa muda wote waliofanya vitendo hivyo .‘’alifafanua Mhandi...

DKT. BITEKO AMWAKILISHA RAIS SAMIA MAZISHI YA HAYATI ASKOFU SHAO

Image
📌 Awataka Watanzania kuacha alama katika utumishi wao 📌 Asema Serikali iko pamoja na wafiwa katika kipindi hiki cha majonzi 📌 Askofu Malasusa ataka waumini kumshuhudia Kristo kwa vitendo Na Ofisi ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amemwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika ibada ya mazishi ya Askofu Mstaafu Dkt. Martin Fatael Shao aliyefariki Dunia Agosti 25, mwaka huu. Akizungumza katika ibada ya mazishi Septemba 4, 2025 yaliyofanyika katika kijiji cha Lole, Wilaya ya Moshi, Mkoani Kilimanjaro Dkt. Biteko amesema Hayati Askofu Shao wakati wa uhai wake alifanya mambo mengi mazuri ya kukumbukwa hata baada ya kifo chake. “ Mzee wetu, Hayati Askofu Shao ameanza kazi za kanisa akiwa kijana na amefanya kazi kubwa ambayo kila mmoja anaishuhudia leo, ameacha alama inayotokana na kazi aliyoifanya, amesema “Mheshimiwa Rais amenituma niwaletee salamu zake za pole nyingi sana Wanafamilia, Viongozi wote wa Ka...

WAKAZI WA KISIWA CHA UKARA, UKEREWE WAIPONGEZA TARURA KWA KUKARABATI BARABARA

Image
Ukara, Ukerewe Wakazi wa Kisiwa cha Ukara wilayani Ukerewe mkoani Mwanza wameishukuru Serikali kupitia Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) kwa hatua ya kuanza kuzikarabati baadhi ya barabara za kisiwa hicho, ambazo kwa muda mrefu zilikuwa zinapitika kwa shida. Wakizungumza wakati wa ziara ya Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI, anayeshughulikia Miundombinu, Mhandisi Rogatus Mativila, wamesema kwa sasa barabara hizo zinapitika bila adha yoyote baada ya TARURA kuzikarabati kwa kiwango cha changarawe. Aidha, wameomba TARURA kuijenga kwa kiwango cha lami barabara ya kutoka darajani kuelekea hospitali ya Bwisya. Kilio cha wakazi wa kisiwa cha Ukara, kinafuatia ahadi za viongozi wakuu wa kitaifa ambao kwa nyakati tofauti wametembelea kisiwa hicho na kuahidi kujenga barabara za Nyamanga-Bwisya, Katende-Bugaramila na Bwisya-Kome zenye jumla ya urefu wa Km 2 kwa kiwango cha lami, ambapo upembuzi yakinifu na usanifu wa barabara hizo tayari umeshafanyika.  

MRADI WA MAJIKO BANIFU WATAMBULISHWA KIGOMA

Image
📌 *Majiko banifu 8,424 kusambazwa na kuuzwa kwa bei ya ruzuku mkoani Kigoma*  📌 *Wilaya Sita kunufaika na mradi*  📌 *Kila Wilaya kupata majiko 1,404*  📍 *KIGOMA*  Wakazi wa Kigoma waaswa kuunga mkono jitihada za Serikali katika utunzaji wa mazingira kwa kutumia nishati safi na salama ya kupikia Wito huo umetolewa leo Septemba 04, 2025 na Mkuu wa Mkoa wa Kigoma Mhe. Simon Nyakoro Sirro wakati akipokea mradi wa uuzaji na usambazaji wa majiko banifu unaosimamiwa na kuratibiwa  na Wakala wa Nishati Vijijini (REA) . "Kinachofanyika leo ni kuunga mkono jitihada za Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan za matumizi ya nishati safi na salama katika kutunza mazingira na kuboresha Afya za wananchi" amesema Mkuu wa mkoa Mhe. Sirro, alipokuwa akipokea mradi huo. Akiwasilisha taarifa ya mradi kwa mkuu wa mkoa, Mhandisi wa Miradi kutoka wakala wa Nishati Vijijini (REA), Raya Majallah amesema, “Mradi huu unalenga kusambaza majiko banifu ili kukuza upatikanaji wa Nishati safi n...

MAKAMU WA RAIS AWEKA JIWE LA MSINGI KITUO CHA MAFUNZO NA MATIBABU YA SARATANI KATIKA HOSPITALI YA BENJAMIN MKAPA*

Image
AZINDUA KITUO CHA HUDUMA ZA UPANDIKIZAJI FIGO KATIKA HOSPITALI YA BENJAMIN MKAPA Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amesema Serikali imedhamiria kuimarisha huduma za tiba za kitalii, ikiwa ni sehemu ya mikakati ya kuboresha na kuimarisha sekta ya afya nchini na kuchangia kwenye Pato la Taifa. Makamu wa Rais amesema hayo wakati wa hafla ya uwekaji wa Jiwe la Msingi Ujenzi wa Kituo cha Mafunzo na Matibabu ya Saratani pamoja na kuzindua Kituo cha Upandikizaji Figo katika Hospitali ya Benjamin Mkapa Jijini Dodoma. Amesema mchango wa Utalii wa Tiba kwenye Pato la Taifa kwa sasa unakadiriwa kuwa Shilingi bilioni 166.5 ambapo idadi wa wagonjwa wanaokuja kutibiwa nchini imeongezeka kutoka 5,700 mwaka 2021 hadi 12,180 mwaka 2025. Makamu wa Rais ametambua mchango wa Hospitali ya Benjamin Mkapa kwa Utalii Tiba, unaotokana na uwekezaji mkubwa uliofanywa na Serikali katika Miundombinu, Vifaa tiba vyenye teknolojia ya kisasa na Wataalamu waliobobea katika maene...