KURA ZOTE BUTINZYA TUMPIGIE DKT. SAMIA - DKT. BITEKO
Mgombea Ubunge wa Jimbo la Bukombe kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Doto Mashaka Biteko amewahimiza wananchi wa Kata ya Butinzya, Wilayani Bukombe kumpigia kura mgombea wa Urais kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi (CCM)Dkt. Samia Suluhu Hassan ili aendelee kuongoza na kusimamia miradi ya maendele iliyokwishaanzishwa na hivyo kuwaletea maendeleo. Dkt. Biteko amesema hayo Septemba 30, 2025 wakati wa mkutano wa kampeni katika Kata ya Butinzya wilayani Bukombe mkoani Geita ikiwa ni sehemu Kampeni za Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani utakaofanyika Oktoba 29, mwaka huu. Amesema wananchi wanalo jukumu la kujotokeza kwa wingi kupiga kura na watakapopiga kura maana yake ni kutimiza wajibu wao kidemokrasia ambao utawawezesha kutimiziwa mahitaji yao kwa kujengewa miradi ya maji, umeme, barabara, hospitali na shule. Amesema katika miaka mitano iliyopita wananchi hao wakishiriki katika kutekeleza miradi ya maendeleo iliyolenga kutatua changamoto za Bukombe na sasa jukumu lililo...