KAMISHNA BADRU AFUNGUA MAFUNZO YA MFUMO MPYA WA MAKAZI ONLINE PORTAL*



📍Arusha | Tarehe 4 Oktoba, 2025.

Kamishna wa Uhifadhi wa Mamlaka ya hifadhi ya eneo la Ngorongoro  Bw Abdul-Razak Badru amefungua mafunzo kwa wadau wa uwekezaji katika sekta ya utalii kuhusu  mfumo mpya wa kidijitali wa Makazi Online Portal (MoPO) kwa lengo la kuongeza uwazi na usawa katika upangaji wa makambi ya kulala wageni (Campsites) hususan eneo la Ndutu Ngorongoro

Akifungua mafunzo hayo Kamishna Badru ameeleza kuwa hatua ya kubuni mfumo mpya wa Makazi Online Portal  inalenga kuboresha huduma kwa wateja katika sekta ya uhifadhi na utalii kwa kujikita kwenye matumizi ya  teknolojia kwa huduma ambazo wadau hao wanazihitaji katika eneo la hifadhi ya Ngorongoro.

“Mfumo tulioubuni kwa dunia ya sasa ni muhimu katika kuboresha huduma kwa misingi ya  uwazi, haki na ufanisi, tunaamini kila mdau atapata huduma nzuri na kwa wakati bila upendeleo,” alisema Kamishna Badru.

Wakati wa mafunzo hayo Wataalam wa TEHAMA na Uwekezaji walitoa semina kwa washiriki kuhusu matumizi ya mfumo wa Makazi Online Portal ikihusisha  namna ya kuomba nafasi za makambi, kufuatilia maombi, na kupata taarifa ya maombi yao kwa wakati.

Mfumo wa Makazi Online Portal uliohudhuriwa na wadau wa uwekezaji katika sekta ya utalii  zaidi ya 150 unatarajiwa kuwa suluhisho la muda mrefu katika kuomba kuwekeza makambi ya kulala wageni eneo la Ndutu  tofauti na mfumo wa zamani wa kutuma barua ya maombi kwa kamishna wa Uhifadhi hali inayoongeza uwazi wa kufuatilia maombi na ufanisi katika upangaji wa kambi hizo.



Comments

Popular posts from this blog

HATMA YA TAIFA IPO KATIKA USAWA WA KIJINSIA, SIO VIWANDA PEKEE.

MSAKO MKALI KUREJESHA HALI ya USALAMA TANGA, WATUHUMIWA 42 WAKAMATWA

PJT-MMMAM YAWEZESHA UANZISHWAJI WA VITUO 206 VYA MALEZI YA WATOTO WADOGO