TARURA YAPATA DOLA MILIONI 65 KUTEKELEZA MIRADI YA DHARURA
#Makandarasi wazawa wanufaika . Tabora Serikali imeiwezesha Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) kupata dola milioni 65 kwa ajili ya utekelezaji wa matengenezo ya miundombinu ya barabara kupitia mfuko wa dharura (CERC). Hayo yamesemwa na Mtendaji Mkuu wa TARURA, Mhandisi Victor Seff wakati wa ziara ya wajumbe wa Bodi ya Ushauri ya Wakala huo katika mradi wa ujenzi wa daraja lenye urefu wa Mita 22 pamoja na barabara za maingilio zenye urefu wa Mita 290 kwenye barabara ya Ndovelwa yenye urefu wa Km. 20.2 katika Manispaa ya Tabora. Mhandisi Seff amesema fedha hizo ni mkopo nafuu kutoka Benki ya Dunia uliotolewa kufuatia tathmini ya uharibifu wa miundombinu uliosababishwa na mvua za El-Nino za mwaka 2024. Amesema tathmini hiyo ilibaini maeneo mengi ya barabara yaliyoharibiwa na hivyo kuhitaji matengenezo ya haraka ili kurejesha mawasiliano na huduma kwa wananchi. “Miradi hii inatekelezwa nchi nzima na kwa wastani utekelezaji wake umefikia asilimia 70. Kazi zote zina...