Posts

Showing posts from April, 2026

RUJAT YATAKA MABADILIKO YA UANDISHI, YAANGAZA ZAIDI VIJIJINI

Image
Na Hamida Ramadhan   Arusha MWENYEKITI  wa Chama cha Waandishi wa Habari za Vijijini Tanzania (RUJAT), Neville Meena, amesema kuwa ni muhimu kuimarisha uhuru wa vyombo vya habari huku ikiwekewa mkazo sauti ya wananchi wa vijijini ili kuhakikisha hakuna kundi linaloachwa nyuma katika upatikanaji wa taarifa. Akizungumza wakati wa maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani yaliyofanyika jijini Arusha, Meena amesema uhuru wa vyombo vya habari unapaswa kuambatana na uwajibikaji wa kitaaluma kwa wanahabari kuzingatia misingi ya ukweli, usahihi, uwiano na maslahi ya umma. Maadhimisho hayo yaliyowakutanisha wadau wa sekta ya habari kwa siku mbili katika Hoteli ya Mount Meru, yalijadili mustakabali wa tasnia ya habari katika muktadha wa mabadiliko ya kidijitali, yakilenga pia kukuza ubunifu na kuhakikisha uendelevu wa taaluma ya uandishi wa habari. Kwa upande wake, Katibu Mtendaji wa RUJAT, Prosper Kwigize, amesema chama hicho kimejipanga kushirikiana na taasisi mba...

TANZANIA YASISITIZA UONGEZAJI THAMANI MADINI NDANI YA AFRIKA*

Image
* ▪️Waziri Mavunde Asisitiza Ushirikiano wa Kikanda  ▪️Ahimiza Uwekezaji Miundombinu ya Kisaaa, Nishati na Sera Rafiki  ▪️Azishauri Serikali Kufanya Kazi kwa Ukaribu na Sekta Binafsi  📍Nairobi, Kenya Serikali ya Tanzania imetoa msimamo thabiti wa kuitaka Afrika kuharakisha mageuzi ya Sekta ya Madini kwa kuwekeza katika uongezaji thamani wa rasilimali zake zikiwemo za madini badala ya kuendelea kuuza madini ghafi yasiyoongeza tija kwa uchumi wa bara hilo. Hayo yameelezwa na Waziri wa Madini wa Tanzania Mhe. Anthony Mavunde wakati akifunga Mkutano wa Kenya Mining Investment Conference & Expo 2026 jijini Nairobi, uliofanyika kwa siku mbili kuanzia Aprili 28 hadi 29, 2026, ambako amesema hatua ya kuchakata madini ndani ya nchi ni nguzo muhimu ya kujenga uchumi wa viwanda na kuongeza ushindani wa Afrika katika soko la dunia. “Afrika haiwezi kuendelea kusafirisha malighafi ghafi na kuagiza bidhaa zilizokamilika. Tunapaswa kujenga uwezo wa kuchakata na kuongeza thamani ya m...

*TAMASHA LA KILIMO LAHITIMISHWA MBEYA* .

Image
📌 *REA Yapongezwa uhamasishaji matumizi ya nishati safi ya kupikia* . 📌 *Umeme sasa ni kitongoji kwa kitongoji*  📍 *Iwambi, Mbeya* . Tamasha la Kilimo lililokuwa likifanyika mkoani Mbeya limehitimishwa rasmi leo Jumatano, tarehe 29 Aprili 2026, kwa mafanikio makubwa huku likiwa limekusanya wadau mbalimbali wa sekta ya kilimo, nishati na maendeleo kutoka ndani na nje ya mkoa huo. Tamasha hilo limekuwa jukwaa muhimu la kubadilishana uzoefu, kuonesha teknolojia mpya na kutoa elimu kwa wananchi kuhusu njia bora za kuboresha maisha yao kupitia kilimo na matumizi sahihi ya nishati. Akizungumza wakati wa hafla ya kufunga tamasha hilo,mgeni rasmi mkuu wa wilaya ya Rungwe Mhe. Jaffar Haniu ameipongeza REA kwa kazi kubwa wanayoifanya ya kuhakikisha wananchi wanapata elimu ya matumizi ya nishati safi, akisisitiza kuwa hatua hiyo ina mchango mkubwa katika kuboresha afya za wananchi na kulinda mazingira. Alieleza kuwa matumizi ya nishati safi kama majiko ya umeme, majiko ya gesi na majiko ba...

WAKALA WA VIPIMO (WMA) YAENDELEA KUTOA ELIMU YA VIPIMO KWA WADAU VIWANJA VYA DKT SAMIA GEITA

Image
 *Elimu ya vipimo ikiendelea kutolewa kwa wadau kutoka Uwanja wa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Geita.*

*REA YATOA ELIMU YA NISHATI SAFI KWA WANANCHI TAMASHA LA KILIMO IWAMBI MBEYA.*

Image
📍 *Iwambi,Mbeya*  Wakala wa Nishati Vijijini (REA) imeendelea kutoa elimu ya matumizi ya nishati safi kwa wananchi katika Tamasha la Kilimo linalofanyika katika viwanja vya Iwambi, mkoani Mbeya. Akizungumza wakati wa tamasha hilo, Mhandisi wa Miradi kutoka REA, Ramadhani Mganga, amesema kuwa lengo la ushiriki wao ni kuwahamasisha wananchi kutumia nishati safi na salama kwa kupikia ili kulinda afya zao na mazingira. Ameeleza kuwa REA inaendelea kusambaza na kuhamasisha matumizi ya teknolojia mbalimbali za nishati safi ikiwemo majiko ya umeme, majiko ya gesi pamoja na majiko banifu, ambayo yanasaidia kupunguza matumizi ya kuni na mkaa. “Ni muhimu kwa wananchi kuelewa faida za nishati safi, si tu katika kulinda mazingira bali pia katika kuboresha afya kwa kupunguza athari za moshi unaotokana na nishati zisizo salama,” amesema Mganga. Aidha, amebainisha kuwa kupitia miradi mbalimbali inayoendelea, upatikanaji wa umeme vijijini umeimarika kwa kiwango kikubwa, hatua inayowezesha wananch...

BUNGE LAPITISHA BIL. 174.9/- KWA WIZARA YA MADINI*

Image
*●Yalenga kuchangia trilioni 1.4/- za maduhuli* *●Makusanyo yafikia Trilioni 1 na Milioni 156* *●Jumla ya tani 23.8 za dhahabu zakusaywa ndani ya miezi 18* *●Ni Juhudi za Rais.Dkt.Samia Suluhu Hassan* *Dodoma* Bunge la Jamhuru ya Muungano wa Tanzania, limeridhia na kupitisha bajeti ya Wizara ya Madini ya shilingi bilioni 174.9 kwa Mwaka wa Fedha 2026/2027 ili kuiwezesha Wizara ya Madini kufanikisha ukusanyaji wa maduhuli ya shilingi trilioni 1.4. Akiwasilisha Bungeni makadirio ya Mapato na Matumizi leo Aprili 27, 2026, Waziri wa Madini, Mhe. Anthony Mavunde amesema fedha hizo zitawezesha kufanikisha utekelezaji wa majukumu ya Wizara pamoja na taasisi zilizo chini yake, huku zikilenga kuendeleza kasi ya ukuaji wa sekta ya madini kwa kufanya tafiti za jiosayansi nchini. Akifafanua mgawanyo wa Bajeti hiyo, Waziri Mavunde amesema kiasi cha  shilingi bilioni 71.5 sawa na asilimia 40.9 zimetengwa kwa ajili ya miradi ya maendeleo, wakati shilingi bilioni 103.5 sawa na asilimia 59.1 zikiwa...

*WAKALA WA NISHATI VIJIJINI (REA) WASHIRIKI TAMASHA LA KILIMO JIJINI MBEYA, WAHAMASISHWA NISHATI SAFI YA KUPIKIA* .

Image
📍 *Iwambi, Mbeya*  Wakala wa Nishati Vijijini (REA) unashiriki katika tamasha la kilimo linalofanyika katika  viwanja vya Iwambi jijini Mbeya kuanzia tarehe 25 mpaka 29 Aprili 2026, ambapo zaidi ya watu 100,000 wakiwemo vijana kutoka mikoa mbalimbali ya kanda ya nyanda za juu kusini wanatarajiwa kushiriki. Wakala unatumia jukwaa hilo kuelimisha na kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa wananchi pamoja na kueleza hali ya upatikanaji wa huduma ya umeme katika maeneo ya vijijini. Kupitia banda lake, REA imeonesha bidhaa mbalimbali za nishati safi ya kupikia, ambapo bidhaa kuu zinazohamasishwa ni pamoja na matumizi ya majiko ya umeme, majiko ya gesi pamoja na majiko banifu. Teknolojia hizo zimebainishwa kuwa suluhisho muhimu katika kupunguza matumizi ya nishati chafu kama kuni na mkaa, kulinda mazingira na kuboresha afya za watumiaji. Akifungua rasmi maonesho hayo, Kaimu mkuu wa wilaya ya Mbeya ambae pia ni Mkuu wa wilaya ya Mbarali Mhe. Brig. jen. Maulid Hassan Suru...

SEKTA YA MADINI YAENDELEA KUONGOZA THAMANI YA MTAJI WA UWEKEZAJI KUTOKA NJE.

Image
Na Deborah Lemmubi-Kipeo Media Dodoma. Wizara ya Madini imesema kuwa Sekta hiyo imeendelea kuongoza katika thamani ya mtaji wa Uwekezaji kutoka nje yani Foreign Direct Investment(FDI) katika mwaka 2024 ikiwa ni takribani ya robo tatu ya jumla ya mtaji wa Uwekezaji katika Sekta muhimu ikitokana na ripoti ya Uwekezaji ya Tanzania ya mwaka 2025. Ambapo pia ripoti hiyo inaonesha kiwango hicho cha mtaji kutoka nje katika Sekta hiyo kiliongezeka hadi kufikia dola bilioni 9.79 mwaka 2024,kutoka dola bilioni 9.15 mwaka 2023 na dola bilioni 8.64 mwaka 2022 ambapo ongezeko limechangiwa na uhamasishaji na uwepo wa mazingira wezeshi kwa wawekezaji. Hayo yamesemwa mapema leo hii Aprili 27,2026 Bungeni Jijini Dodoma na Waziri wa Madini Mhe Anthony Peter Mavunde wakati akiwasilisha Makadirio ya mapato na matumizi kwa mwaka wa Fedha wa 2026/2027. "Mhe Spika, Kulingana na ripoti ya uwekezaji Tanzania ya mwaka 2025(Tanzania Investement Report 2025) Sekta ya Madini imeendelea kuongoza katika thamani...

DC RUKIA ATEMBELEA MIUNDOMBINU YA TANESCO NA SAMWASA

Image
DC RUKIA ATEMBELEA MIUNDOMBINU YA TANESCO NA SAMWASA. Mwanga, Kilimanjaro.  Mkuu wa Wilaya ya Mwanga mkoani Kilimanjaro Bi. Rukia Zuberi akiwa ameambatana na viongozi wengine ngazi ya wilaya, wamefanya ziara kwenye miundombinu ya umeme iliyo chini ya Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) na Mamlaka ya Maji Safi na Usafi wa Mazingira Same-Mwanga (SAMWASA) kwa lengo la kuona hali halisi ya utendaji kazi, kujadili na kushauriana ili kuboresha huduma kwa wananchi. Akieleza lengo la ziara hiyo, Mkuu wa Wilaya, Bi. Rukia Zuberi, amesema ni kuona hali halisi ya utendaji, kujadili na kushauriana namna ya kukabiliana changamoto zinazozikabili taasisi hizo, ili ziweze kuendelea kutoa huduma bora na zenye tija kwa wananchi. Akiwa katika ofisi hizo, alipata maelezo kutoka kwa watumishi kuhusu mifumo ya kazi, utoaji wa huduma kwa wateja pamoja na changamoto mbalimbali zinazojitokeza katika sekta za umeme na maji, huku akielezwa juhudi zinazofanyika kuboresha huduma hizo. Hata hivyo amesisitiza ut...

SERIKALI YAIMARISHA UWAZI SEKTA YA MADINI, BEI ELEKEZI KUTOLEWA KILA SIKU

Image
KAHAMA Serikali kupitia Tume ya Madini imesema itaendelea kutoa bei elekezi za madini ya dhahabu, shaba na fedha kila siku itakayotumika kwenye masoko na vituo vya ununuzi wa madini hatua inayolenga kuongeza uwazi katika biashara ya madini na kuwawezesha wachimbaji kuuza madini yao kwa bei halisi ya soko la dunia. Akifunga mafunzo kwa Mameneja na Wakaguzi Wakuu wa Migodi ya uchimbaji mdogo kutoka mikoa ya kimadini ya Kahama, Mbogwe na Shinyanga mapema jana, Mkurugenzi wa Ukaguzi na Biashara ya Madini, CPA Venance Kasiki alisema taarifa hizo za bei zitawasaidia wachimbaji kufanya maamuzi sahihi ya biashara na kuepuka hasara zitokanazo na madalali maarufu kama vishoka. Alisema hapo awali baadhi ya wachimbaji walikuwa wakiuza madini bila kufahamu bei halisi ya soko la dunia, hali iliyosababisha kupoteza mapato na kuingia katika mikataba isiyo na manufaa.  Alifafanua kuwa kwa sasa bei za madini hutolewa kila siku, hivyo mchimbaji ana uwezo wa kufanya uamuzi sahihi kabla ya kuuza madini...

TARURA YAWAJENGEA UWEZO WATAALAM WAKE KUHUSU USIMAMIZI WA MRADI SANIFU NA JENGA

Image
‎ ‎Arusha ‎ ‎Mtendaji Mkuu wa Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) Mhandisi Victor Seff, amefungua mafunzo ya siku tatu yenye lengo la kuwajengea uelewa wataalamu wa TARURA kutoka TAMISEMI, ofisi ya Makao Makuu, Mikoa, Wilaya, Mhandisi Mshauri pamoja na Mkandarasi katika kutekeleza mradi wa Sanifu na Jenga wa barabara zinazoingia uwanja wa AFCON jijini Arusha. ‎ ‎Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, Mhandisi Seff alisema lengo kuu ni kujenga uelewa wa pamoja kuhusu utekelezaji wa miradi ya sanifu na jenga ili kuimarisha uzingatiaji wa taratibu, kushughulikia changamoto kwa wakati na kuhakikisha mradi unatekelezwa kwa mafanikio. ‎ ‎Alifafanua kuwa mafanikio hayo yanapaswa kuzingatia misingi ya usalama, masuala ya kijamii na kimazingira, muda, gharama, thamani, ubora pamoja na mahitaji ya kiutendaji. ‎ ‎Mhandisi Seff alibainisha kuwa tangu kuanzishwa kwa TARURA, Wakala huo haujawahi kupata mradi mkubwa kama huo, hivyo mafunzo hayo ni fursa muhimu ya kuwajengea uwe...

WANANCHI CHUNYA KUNUFAIKA NA MRADI WA MAJIKO BANIFU KWA BEI YA RUZUKU*

Image
  📌 *Majiko 1,555 kuuzwa kwa bei ya ruzuku*  📌 *Serikali kutoa ruzuku ya asilimia 85 kwa kila jiko* . 📍 *Chunya, Mbeya*  Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Chunya ambaye pia ni Mwanasheria Mkuu wa halmashauri hiyo, Wakili Athumani Bamba leo Aprili 24, 2026 amezindua rasmi mradi wa usambazaji na uuzaji wa majiko banifu kwa bei ya ruzuku katika mji mdogo wa Makongolosi, wilayani Chunya mkoani Mbeya. Akizungumza katika hafla ya uzinduzi huo, Kaimu Mkurugenzi huyo alisema mradi huo unalenga kuwapatia wananchi nishati mbadala iliyo nafuu, salama na rafiki kwa mazingira, huku ukichochea kupunguza matumizi makubwa ya kuni na mkaa ambao umeendelea kuwa chanzo cha uharibifu wa misitu. Alieleza kuwa kupitia mpango huo wa ruzuku, wananchi wataweza kumudu kununua majiko banifu kwa gharama nafuu zaidi, jambo litakalosaidia kupunguza matumizi ya nishati zisizo rafiki pamoja na kuboresha afya za watumiaji kwa kupunguza athari za moshi majumbani. “Ni muhimu wananchi wakautum...

_MAKAMU WA RAIS AWEKA JIWE LA MSINGI UJENZI WA MAABARA YA SAYANSI NA SKULI YA KILIMO YA CHUO KIKUU CHA TAIFA CHA ZANZIBAR*

Image
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Balozi Dkt. Emmanuel Nchimbi amesema mradi wa ujenzi wa Maabara za Sayansi na Skuli ya Kilimo ya Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA) ni muhimu kwa kuwa unaolenga kuweka misingi imara ya maendeleo ya Teknolojia, Ujuzi, na Uchumi katika jamii.   Makamu wa Rais amesema hayo wakati akiweka Jiwe la Msingi la ujenzi wa Maabara za Sayansi na Skuli ya Kilimo ya Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar (SUZA) ikiwa ni shamrashamra za Miaka 62 ya Muungano. Amesema mradi huo utaleta manufaa makubwa kwa nchi, ikiwa ni pamoja na kutengeneza fursa za ajira, kuongeza uelewa katika sayansi na teknolojia, kushajihisha uchumi wa buluu na kuongeza tija katika kilimo.   Aidha, Makamu wa Rais amesema elimu ni kipaumbele cha Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwa ndiyo inayowezesha uendelezaji wa rasilimaliwatu ili kuchangia kikamilifu katika kujenga Taifa na kuleta maendeleo kwa ujumla. Ameongez...

*BUNGE LAPITISHA KWA KISHINDO BAJETI YA WIZARA YA NISHATI 2026/2027*

Image
📌*Ni shilingi trilioni 2.53* 📌*Serikali kuja na mradi wa kuunganisha umeme kwa sh.27,000 katika maeneo ya Mjini yenye sura ya Vijiji* 📌*Mradi wa kuzalisha umeme megawati 2000 kwa makaa ya mawe mbioni* Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania limepitisha kwa kishindo shilingi trilioni 2.53 kwa ajili ya matumizi ya Wizara ya Nishati 2026/2027. Kati ya fedha hizo, Shilingi trilioni 2.46 sawa na asilimia 97.5 ya bajeti yote  imeelekezwa kwenye miradi ya maendeleo na asilimia 2.5 ni kwa ajili ya matumizi ya kawaida. Akihitimisha hoja kuhusu makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya Nishati kwa mwaka 2026/2027 Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi alilieleza Bunge kuwa Wizara ya Nishati itaendelea kuhakikisha kwamba maono ya Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, maelekezo ya Ilani ya Chama cha Mapinduzi na mwelekeo uliowekwa kwenye Dira 2050 yanatekelezwa kwa vitendo na kwa haraka. Kutokana na hilo alieleza kuwa lengo lililowekwa kwa Wizara la kuzalisha umeme  wa megawati...

*WIZARA YA NISHATI YAPONGEZWA KUONDOA UTEGEMEZI WA FEDHA ZA NJE KATIKA MIRADI*

Image
Mbunge wa Jimbo la Itilima, Njalu Silanga (CCM) amepongeza hatua ya Wizara ya Nishati kupunguza utegemezi wa fedha kutoka nje katika utekelezaji wa miradi ya sekta ya nishati. Akichangia hotuba ya makadirio ya mapato na matumizi ya Wizara ya.Nishati  na Taasisi zake kwa mwaka 2026/27, Silanga amesema hatua hiyo inatoa uhakika wa utekelezaji wa miradi ya nishati ambayo ni mhimili mkuu katika ukuaji wa uchumi. Wizara ya Nishati imeomba kuidhinishiwa Sh trilioni 2.53 kwa ajili ya matumizi ya wizara na taasisi zake kwa mwaka wa fedha 2026/27, kati ya fedha hizo, Sh trilioni 2.46 sawa na asilimia 97.5 ya bajeti yote ya wizara zimeelekezwa kwenye miradi ya maendeleo.  Kati ya fedha za maendeleo zilizoombwa, Sh trilioni 1.6 ni fedha za ndani, huku Sh bilioni 859.92 zikiwa fedha za nje.