TARURA YATEKELEZA UJENZI WA KM 56 ZA BARABARA ZA LAMI ILALA KUPITIA DMDP II
Dar es Salaam Serikali kupitia Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) imeanza kutekeleza ujenzi wa barabara zaidi ya Kilomita 56 kwa kiwango cha lami na zege kupitia mradi wa Uendelezaji Jiji la Dar es Salaam Awamu ya Pili (DMDP II) katika Halmashauri ya Manispaa ya Ilala mkoani humo. Akiwa katika ziara ya ukaguzi wa miradi hiyo Kaimu Meneja wa TARURA wilaya ya Ilala, Mhandisi Grayson Nzunda amesema kuwa miradi inayojengwa ni barabara za lami na zege, mifereji ya maji ya mvua, makalavati, njia za waenda kwa miguu, uwekaji wa taa za barabarani pamoja na kuweka alama za barabarani ambapo mradi unagharimu shilingi Bilioni 138. “Hapa tulipo ni maeneo ya Kivule tupo kukagua ujenzi wa barabara zenye urefu wa Kilomita 12, barabara ya Kivule-Majohe Junction Km 2.79 inajengwa kwa kiwango cha zege na barabara ya Kitunda-Kivule-Msongola Km 9.95 inajengwa kwa kiwango cha lami, mradi umegharimu shilingi Bilioni 30 kati ya Bilioni 138 za wilaya nzima ya Ilala", ...