Posts

Showing posts from June, 2026

MTAKUWWA YAZINDUA KAMPENI Ya 'AMSHA ARI' MIRONGO KUHAMASISHA KUPINGA UKATILII KWA WANAWAKE NA WATOTO

Image
  Mwanza. Kamati ya Ulinzi na Usalama wa Wanawake na Watoto Mkoa wa Mwanza (MTAKUWWA) imezindua kampeni ya Amsha Ari katika Kata ya Mirongo, ikiwa na lengo la kuhamasisha jamii kushiriki katika malezi bora ya watoto, kuzuia mmomonyoko wa maadili na kutokomeza vitendo vya ukatili dhidi ya wanawake na watoto. Uzinduzi wa kampeni hiyo uliwashirikisha waendesha bodaboda wa Kata ya Mirongo, ambao walieleza utayari wao wa kushiriki kikamilifu katika kuelimisha jamii kuhusu madhara ya ukatili dhidi ya wanawake na watoto pamoja na kuhamasisha ulinzi wa makundi hayo. Aidha, waendesha bodaboda hao waliitaka jamii kuendelea kudumisha amani iliyopo nchini na kuwahimiza vijana kuepuka kutumika katika vitendo vya uchochezi vinavyoweza kuhatarisha usalama wa wananchi na mali zao. Akizungumza katika uzinduzi huo, Mwenyekiti Mwenza wa MTAKUWWA Mkoa wa Mwanza, Yassin Ally, aliwataka waendesha bodaboda kuwa mstari wa mbele katika kufichua vitendo vya ukatili, kutoa elimu kwa jamii kuhusu athari zake ...

RAIS DKT.SAMIA S. HASSAN KUFUNGUA MKUTANO MKUBWA WA MADINI NOVEMBA 2026*

Image
-▪️Ni Mkutano mkubwa wa Madini na Uwekezaji ▪️Washiriki 2000 kutoka mataifa 50 Duniani kushiriki ▪️Kauli Mbiu ya Mkutano inalenga kuongeza thamani madini kwa maendelezo ya Viwanda ▪️Serikali na Sekta Binafsi kushirikiana kuandaa mkutano huo ▪️Waziri Mavunde azindua rasmi maandalizi ya mkutano huo 📍 DAR ES SALAAM.  Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt. Samia S. Hassan anatarajiwa kufungua rasmi Mkutano wa Saba wa Madini na Uwekezaji Tanzania (TMIC 2026) utakaofanyika Novemba 19 hadi 21, 2026 katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano cha Julius Nyerere (JNICC), Dar es Salaam. Akizungumza leo Juni 27, 2026 wakati wa uzinduzi wa TMIC 2026, Waziri wa Madini, Anthony Mavunde, amesema serikali imeamua kujenga uchumi wa viwanda unaotokana na madini kwa kuwekeza katika uchakataji na uyeyushaji wa madini badala ya kuendelea kuuza malighafi. Amesema kaulimbiu ya mkutano huo, "Madini Yaliyoongezwa Thamani: Chachu ya Ukuaji wa Viwanda na Uchumi," inaakisi dira ya serikali ya kui...

*MHE. SALOME AHAMASISHA MATUMIZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA KUPITIA MARATHON*

Image
Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, leo Juni 27, 2026 ameshiriki Mbio za Nishati Safi ya Kupikia (Clean Cooking Marathon) zilizofanyika katika Viwanja vya St. Peters Oysterbay jijini Dar es Salaam, ikiwa ni sehemu ya kampeni ya kitaifa ya kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini. Akizungumza wakati wa kufungua mbio hizo, Mhe. Salome amesema pamoja na hatua nzuri iliyofikiwa, matumizi ya nishati safi ya kupikia nchini bado yako katika kiwango cha asilimia 28.6, hali inayoonesha kuwa bado kuna kazi kubwa ya kufanya ili kufikia lengo la asilimia 80 ya matumizi ya nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034. Amesema mbio hizo si mashindano ya kawaida ya kutafuta medali au vikombe, bali ni chachu ya mabadiliko ya kifikra na kijamii yanayolenga kulinda afya za wananchi, kuhifadhi mazingira na kuwawezesha wananchi kiuchumi, huku akisisitiza kuwa Serikali itaendelea kutekeleza Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia wa mwaka 2024–2034 unaolenga kuhakikish...

MWENGE WA UHURU WAKABIDHI GARI LA WAGONJWA LUSHOTO

Image
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Bw. Wazo Mwang'onda, amekabidhi gari jipya la kubebea wagonjwa kwa Hospitali ya Wilaya ya Lushoto, akisema hatua hiyo ni sehemu ya juhudi za Serikali ya Awamu ya Sita za kuimarisha huduma za afya na kuwafikisha wananchi huduma muhimu kwa wakati. Akizungumza wakati wa mapokezi ya Mwenge wa Uhuru yaliyofanyika katika viwanja vya Shule ya Msingi Kizala, wilayani Lushoto, Bw. Mwang'onda amesema ujio wa gari hilo unaonesha dhamira ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ya kuendelea kuboresha sekta ya afya kupitia ujenzi wa vituo vya afya, zahanati pamoja na upatikanaji wa magari ya wagonjwa katika maeneo mbalimbali nchini. Kwa upande wake, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu – TAMISEMI na Mbunge wa Jimbo la Lushoto, Prof. Riziki Shemdoe, amemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kuwapatia wananchi wa Lushoto gari hilo, akieleza kuwa litasaidia kwa kiwango kikubwa kuboresha huduma za rufaa kwa wagonjwa wanaohitaji usafiri wa haraka kwenda k...

*SERIKALI IMEDHAMIRIA KULETA MAPINDUZI YA NISHATI SAFI YA KUPIKIA - NAIBU WAZIRI SALOME*

Image
📌Imepunguza kodi kwenye vifaa vya Nishati Safi 📌Lengo ni kuwafikia wananchi wa aina zote. Imeelezwa kuwa Serikali  ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imeweka dhamira  ya dhati  katika kuleta  mapinduzi ya matumizi ya Nishati  Safi ya kupikia yanayoongozwa na mkakati wa taifa wa Nishati Safi ya kupikia  kwa mwaka 2024-2034 unaolenga kuhakikisha asilimia 80 ya watanzania wanatumia Nishati Safi ya kupikia ifikapo 2034. Ameyasema hayo Naibu Waziri wa Nishati  Mhe. Salome Makamba alipokuwa akifunga kongamano la kuhamasisha na kuelimisha juu ya matumizi ya Nishati  safi ya kupikia Juni 25, 2026 lilokuwa likifanyika katika Ukumbi  wa East  Africa Commercial Logistic Center uliopo Jijini  Dar es Salam. Mhe. Salome amesema kuwa ni muda wa kuhakikisha kila mtanzania ananufaika na matumizi ya Nishati Safi  ya Kupikia ili kuweza kulinda afya pamoja na kutunza Mazingira hali itakayosaidia Nchi kuingia kwenye mapinduzi  makubwa ya Mat...

RC MTANDA AAGIZA MPANGO WA KUPUNGUZA MADENI YA WAZABUNI NA WATUMISHI MAGU

Image
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda amesema Baraza la Madiwani linapaswa kufahamu madeni yote ya wazabuni na watumishi ili kuweka mpango wa kuyapunguza hatua kwa hatua katika miaka ijayo. Mhe. Mtanda ametoa kauli hiyo leo Juni 25, 2026, alipokuwa akizungumza katika Mkutano Maalumu wa Baraza la Madiwani wa kujadili hoja za Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa Halmashauri ya Wilaya ya Magu. Amesema ni muhimu kutambua wazabuni wanaodaiwa pamoja na kiasi wanachodai ili halmashauri iweze kuandaa mkakati wa malipo utakaosaidia kupunguza madeni hayo ndani ya kipindi cha miaka miwili hadi mitatu. Aidha, ameeleza kuwa watumishi wanaoidai halmashauri wanapaswa kubainishwa pamoja na madai yao ili kuwepo mpango maalumu wa kulipa madeni hayo kwa awamu na hivyo kupunguza mzigo wa kifedha. Mkuu huyo wa Mkoa pia amesisitiza kuwa fedha zote za Serikali zinazodaiwa lazima zirejeshwe, akizitaka halmashauri zote za Mkoa huo kuunda timu maalumu (task force) za kufuatilia na kukusanya madeni yot...

*MHE. SALOME AZINDUA MFUMO WA KUAGIZA GESI YA KUPIKIA KIDIJITALI*

Image
📌*Unalenga kurahisisha upatikanaji wa nishati safi ya kupikia kwa wananchi* Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba, amezindua mfumo wa kidijitali wa kuagiza gesi ya kupikia uitwao Orion Gas, unaomilikiwa na kampuni ya Hygge, utakaowezesha wateja kuagiza mitungi ya gesi mtandaoni na kufikishiwa bila gharama za usafirishaji.  Mfumo huo utaanza kutumika katika mkoa wa Dar es Salaam kama sehemu ya kurahisisha upatikanaji wa nishati safi ya kupikia kwa wananchi. Akizungumza Juni 25, 2026 wakati akifunga Maonesho na Kongamano la Nishati Safi ya Kupikia yaliyofanyika katika Ukumbi wa EACLC, Ubungo jijini Dar es Salaam, Mhe. Salome  amesema Serikali chini ya uongozi wa Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, imeweka mkazo mkubwa katika utekelezaji wa Mkakati wa Taifa wa Matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia wa mwaka 2024–2034 unaolenga kuhakikisha asilimia 80 ya Watanzania wanatumia nishati safi ya kupikia ifikapo mwaka 2034. Amesema Serikali imeendelea kuchukua hatua mbalimbali za ...

*SALOME MAKAMBA AFUNGA MAONYESHO YA NISHATI EXPO 2026*

Image
📌*Apongeza juhudi za REA kusambaza Nishati Safi ya kupikia vijijini* 📍Dar es Salaam Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Salome Makamba leo tarehe 25 Juni, 2026 amefunga rasmi Maonesho na Kongamano la Nishati Safi Expo 2026  yaliyofanyika katika ukumbi wa EACLC jijini Dar es Salaam Akiwa katika banda la Wakala wa Nishati Vijijini (REA), ameipongeza REA kwa kuendelea kusambaza na kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia hususan katika maeneo ya vijijini na pembezoni mwa miji.  "Naipongeza REA kwa kazi kubwa mnayoifanya katika kuimarisha upatikanaji wa nishati safi ya kupikia na naendelea kuwahimiza wananchi kuendelea kutumia teknolojia mpya za nishati safi ili kulinda afya, mazingira na kuboresha ustawi wa jamii, " Ameongeza Mhe. Makamba.  Amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kuwekeza na kushirikiana na wadau mbalimbali ili kuhakikisha malengo ya Taifa ya matumizi ya nishati safi ya kupikia yanafikiwa kwa manufaa ya Watanzania wote. Aidha, Mhe. Makamba ameelezwa hatua mb...

MTAKUWWA YAANZA OPERESHENI YA MALEZI BORA NA ULINZI WA WATOTO MWANZA

Image
Kamati ya Ulinzi na Usalama wa Wanawake na Watoto Mkoa wa Mwanza (MTAKUWWA) imezindua kampeni ya “Amsha Ari” yenye lengo la kuhamasisha malezi bora, kuzuia mmomonyoko wa maadili na kutokomeza ukatili dhidi ya wanawake na watoto mkoani Mwanza. Akizungumza wakati wa uzinduzi wa kampeni hiyo uliofanyika katika Soko la Milongo, Mwenyekiti Mwenza wa MTAKUWWA Mkoa wa Mwanza, Yassin Ally, amesema kampeni hiyo itatekelezwa kwa mfumo wa nyumba kwa nyumba, mtaa kwa mtaa na pango kwa pango ili kuwafikia wananchi wengi zaidi. Amesema baadhi ya maeneo hayo yamekuwa hatarishi kwa malezi ya watoto, hivyo kampeni hiyo imelenga kufikia makundi mbalimbali ya jamii kupitia mbinu tofauti za utoaji elimu na uhamasishaji. Kwa upande wao, wajumbe wa MTAKUWWA Mkoa wa Mwanza ambao ni viongozi wa dini, wameitaka jamii, hususan waumini wao, kuzingatia malezi bora ya watoto na kujiepusha na vitendo vya ukatili wa kijinsia dhidi ya wanawake na watoto. Wakizungumza kwa nyakati tofauti, wafanyabiashara wa Soko la Mi...

*CHUO CHA DHOW COUNTRIES MUSIC ACADEMY CHA ZANZIBAR CHASHINDA TUZO YA UNESCO-SHARJAH YA UTAMADUNI*

Image
Paris, Ufaransa Chuo cha Dhow Countries Music Academy (DCMA) cha Zanzibar kimeandika historia baada ya kutangazwa mshindi wa Tuzo ya 21 ya UNESCO-Sharjah Prize for Arab Culture, katika hafla iliyofanyika Makao Makuu ya UNESCO jijini Paris, Ufaransa. Chuo hicho kimetunukiwa tuzo hiyo kutokana na mchango wake mkubwa katika kuhifadhi, kufundisha na kuendeleza urithi wa muziki wa taarab na tamaduni za ukanda wa Bahari ya Hindi na Kiarabu.   Mwakilishi wa chuo hicho, Bi. Haldah Am Al-Kanaan, alikuwepo Paris kupokea tuzo hiyo kwa niaba ya taasisi. DCMA ni chuo pekee cha muziki Zanzibar kinachojikita katika kufundisha ala za asili na mitindo ya muziki wa jadi ikiwemo taarab, kidumbak na ngoma, huku kikileta pamoja wanafunzi kutoka mataifa mbalimbali na rika tofauti.   Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa UNESCO, Profesa Khaled El-Enany, alikipongeza chuo hicho kwa ubunifu wake katika kuhifadhi na kuendeleza urithi wa muziki wa Kiarabu na Kiswahili. Alisema m...

RC MTANDA AWATAKA MISUNGWI DC KUSHIRIKIANA KUWALETEA MAENDELEO WANANCHI

Image
Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Mhe. Said Mtanda ameitaka halmashauri ya wilaya ya Misungwi kuimarisha umoja baina ya Baraza la Madiwani na Menejimenti kuwaletea wananchi huduma bora za kijamii kwa kutumia mapato ya ndani kwa kujenga shule, vituo vya afya na miundombinu ya maji. Mhe. Mtanda amefikia hatua ya kutoa agizo hilo baada ya kubaini uwajibikaji duni kwenye ukusanyaji kwa mwenendo wa miaka mitatu na udhaifu kwenye kujibu hoja ambapo kwa mwaka husika wa fedha hoja 81 zimetekelezwa 23 pekee sawa na asilimia 28.4 huku hoja 57 bado hazijajobiwa sawa na asilimia 70.4. Ametoa agizo hilo leo tarehe 24 juni, 2026 wakati akihutubia Mkutano Maalumu wa Baraza la Madiwani wa kujadili hoja za Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) pamoja na Maagizo ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (LAAC) 2024/25 ambapo wamepata hati safi. "Maendeleo ya Misungwi yanawategemea ninyi viongozi na watendaji mlioaminiwa hapa, mkileta mzaha kwenye uwajibikaji mtasababisha halmashauri hi...