MFUMO WA BIASHARA YA MADINI TANZANIA WAIVUTIA UGANDA

MFUMO WA BIASHARA YA MADINI TANZANIA WAIVUTIA UGANDA Na Mwandishi Wetu. Dodoma. Wizara ya Madini na Fedha ya Jamhuri ya Uganda imeonesha kuvutiwa na namna Tanzania inavyoendesha shughuli za biashara ya madini, hususan mfumo wa masoko unaotumika nchini, ikilenga kuboresha mifumo yao kwa kutumia uzoefu wa Tanzania kama mfano wa mafanikio. Hayo yamebainishwa leo Julai 31, 2025 jijini Dodoma wakati wa ziara ya ujumbe kutoka Uganda uliofika katika Wizara ya Madini ya Tanzania ukiongozwa na Kamishna wa Madini wa Uganda Agnes Alabai kwa madhumuni ya kujifunza kuhusu mfumo wa usimamizi na uendeshaji wa biashara ya madini pamoja na masoko ya madini nchini Tanzania. Pia, ameipongeza Wizara ya Madini kwa kuwapatia mafunzo na taarifa mbalimbali zinazolenga kuboresha ufanisi wa sekta ya madini kwa kuzingatia uwazi bila kuficha taarifa yoyote. Alabai amesema ziara hiyo imekuwa ni sehemu ya juhudi za Uganda kuimarisha sekta yake ya madini kwa kuiga mifumo yenye mafanikio kutoka mataifa jirani. K...