*CHANDA CHEMA HUVIKWA PETE*
Maafisa na askari wa jeshi la Uhifadhi wa Mamlaka ya Hifadhi ya eneo la Ngorongoro waliopoteza maisha, kujeruhiwa na kufanya kazi kwa uhodari wametunukiwa vyeti na fedha kutokana na kujitoa kwao kwa hali na mali kulinda rasilimali za wanyamapori na misitu. Tuzo hizo zimetolewa tarehe 31 Julai 2026 kwenye maadhimisho ya siku ya askari wanyamapori duniani ambayo huadhimishwa kwa lengo la kuutambua mchango wa askari hao katika kulinda rasilimali za nchi na kuenzi mchango wa Askari 10 waliopoteza maisha yao na kujeruhiwa wakiwa kazini katika hifadhi ya Ngorongoro. Naibu kamishna wa Uhifadhi huduma za shirika Aidan Makala amewapongeza askari wote wa jeshi la uhifadhi kutokana na kujitoa kwa hali na mali katika kazi hiyo huku akiwasisitiza kufanya kazi kwa kushirikiana na wananchi ili kulinda matakwa ya haki jinai. Naibu Kamishna Makala ameleza kuwa, askari wa uhifadhi ni nguzo ya ulinzi wa rasilimali za wanyamapori na misitu ambapo...