Posts

Showing posts from June, 2025

WATAALAM SADC WAKUTANA ZIMBABWE KUJADILI SEKTA YA NISHATI NA MAJI

Image
📌 *Miundombinu ya usafirishaji umeme kikanda kujadiliwa* 📌 *Nishati Safi ya kupikia kupewa kipaumbele* 📌 *Mkakati mahsusi wa kuongeza watumiaji wa umeme Afrika (M300) kuwa moja ya Ajenda* 📌 *Maendeleo ya Sekta ndogo ya Mafuta na Gesi pamoja na umeme vijijini kujadiliwa* Wataalam wa Wizara ya Nishati pamoja na taasisi zake  leo wameshiriki katika Mkutano wa ngazi ya  Makatibu Wakuu na Watalaam wanaoshughulikia masuala ya Nishati na Maji unaofanyika katika Jiji la Harare nchini Zimbabwe.  Mkutano huo wa awali ni sehemu ya maandalizi kuelekea katika Mkutano wa pamoja wa Kamati ya Mawaziri wanaoshughulikia masuala ya Nishati na Maji wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC).  Mkutano huo pamoja na kujadili masuala ya Nishati na Maji, umekuwa ni fursa pia kwa Tanzania  kuendeleza diplomasia ya kiuchumi pamoja na kuwasilisha mafanikio ya nchi katika kuboresha huduma za nishati vijijini kupitia miradi inayotekelezwa na Wakala wa Nishati Vijijjni (REA). ...

WAZIRI GWAJIMA AZINDUA MADAWATI YA HUDUMA ZA USTAWI JAMII KATIKA VITUO VYA USAFIRISHAJI.

Image
Na WMJJWM - Dar Es Salaam Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum Mhe. Dkt. Dorothy Gwajima amezindua rasmi Mwongozo wa Taratibu za Utoaji wa Huduma za Ustawi wa Jamii kwa Watoto Wanaoishi na Kufanya Kazi Mitaani pamoja na Dawati la Huduma katika Stendi ya Mabasi ya Magufuli Juni 30, 2025 Jijini Dar Es Salaam. Amesema kuwa Serikali ya Awamu ya Sita imejipanga kwa vitendo kukomesha tatizo la watoto wanaokimbilia mitaani kutokana na changamoto za kifamilia, kiuchumi na kijamii. Amesema takwimu zilizotolewa zinaonesha kuwa zaidi ya watoto 10,000 waliokolewa kati ya Julai 2024 hadi Juni 2025 kupitia kampeni maalum ya kitaifa. Mwongozo huo utasaidia watoa huduma kwenye vituo vya usafiri kubaini viashiria vya hatari kama vile ukatili usafirishaji haramu na utoroshwaji wa watoto mapema, hivyo kuwaokoa kabla hawajazama katika maisha ya mitaani. "Mtoto hana mtaa  hivyo anapaswa kuwa mikononi mwa familia na jamii yake. Tuungane kwa dhati kumaliza tatizo hili kwa vit...

BALOZI CHANA AWAVISHA VYEO MANAIBU KAMISHNA WAWILI NA KUSHUHUDIA UVISHWAJI VYEO WA MAKAMISHNA WASAIDIZI WAANDAMIZI WATANO WA NCAA.

Image
Kassim Nyaki, NCAA Arusha. Waziri wa Maliasili na Utalii Balozi Dkt. Pindi Chana (Mb) amewavisha cheo manaibu kamishna wawili na kushuhudia uvishwaji vyeo kwa makamishna wasaidizi waandamizi watano waliovishwa vyeo na mwenyekiti wa bodi ya Wakurugenzi NCAA Jenerali Venance Mabeyo (Mstaafu) Waliovishwa Cheo na Mhe. Waziri ni Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi Joas John Makwati aliyepandishwa cheo kuwa Naibu Kamishna wa Uhifadhi anayesimamia Uhifadhi, utalii na Maendeleo ya Jamii na Naibu Kamishna wa Uhifadhi Aidan Paul Makalla anayesimamia Huduma za Shirika NCAA. Kwa upande wa makamishna waliovishwa vyeo na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi NCAA Jenerali Venance Mabeyo (mstaafu) ni Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi anayesimamia idara ya Mipango na uwekezaji, Gasper Stanley Lyimo, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi Paul Geofrey Shaidi anayesimamia Kitengo cha huduma za Sheria, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Uhifadhi Charles Marwa Wangwe anayesimamia Idara ya Uhasibu n...

KAMISHNA BADRU ALA KIAPO CHA MAADILI.*

Image
Kamishna wa Uhifadhi, Mamlaka ya Hifadhi ya eneo la Ngorongoro (NCAA), Bw. Abdul-Razaq Badru leo tarehe 28 Juni, 2025 ameungana na viongozi wengine walioteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungaano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kula Kiapo cha Maadili katika hafla iliyofanyia Ikulu Chamwino Dodoma. Akitoa ujumbe wake mara baada ya kuwaapisha viongozi wateule, Rais, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amemtaka Kamishna Badru kusimamia kikamilifu shughuli za Uhifadhi, kulinda Ikolojia, Uwekezaji na Maendeleo ya Jamii.  Dkt Samia amesema Ngorongoro ni Urithi wa Dunia hivyo ni lazima ilindwe kuhakikisha kwamba ikolojia yake inaimarishwa na kulinda rasilimali zilizopo na kuhakikisha kuwa  umaarufu wake haupotei.  Amesema ana matumaini makubwa na Kamishna Badru kutumia maarifa yake, ujuzi na uzoefu wake katika kuisimamia Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro. Rais Samia  alimteua Bw. Abdul-Razaq Badru kuwa Kamishana wa Uhifadhi NCAA tarehe 26 Mei, 2025  

WAZIRI MCHENGERWA AWAFUNDA MA RC WAPYA*

Image
Na John Mapepele  Mara baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwaapisha na kutoa maelekezo kwa viongozi kadhaa aliowateua ikiwa ni pamoja na Wakuu wa Mikoa, Waziri wa TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa amekutana na kuwafunda. Mhe. Mchengerwa amewataka kuzingatia maelekezo yote waliyopatiwa na Mhe. Rais huku akisisitiza kuwa wanatakiwa kuwatumikia wananchi kwa kuwa Serikali ni ya wananchi na wasisite kuwasiliana na Wizara wapatapo changamoto. "Ndugu zangu nadhani mmeiona dhamira ya Mhe. Rais ya kuwataka kwenda kuwatumikia wananchi.Mimi siwezi kuongeza chochote nawaombeni mkayazingatie yale yote aliyowaelekeza" amesisitiza Mhe Mchengerwa  Katika hotuba yake baada ya kuwaapisha  Wakuu wa Mikoa hao wapya  Mhe. Rais ametoa maelekezo mahususi  manne ikiwa ni pamoja na kuwataka  kutunza amani na usalama wa  wananchi katika mikoa yao kwa kuzingatia  kuwa Tanzania inakwenda kwenye uchaguzi mkuu Oktoba mwaka huu....

WACHIMBAJI WA SHABA WAASWA KUJIUNGA VIKUNDI KUNUFAIKA NA FURSA ZA MAENDELEO*

Image
Mpwapwa, Dodoma – Juni 28, 2025_ Wachimbaji wadogo wa madini ya shaba wilayani Mpwapwa mkoani Dodoma wametakiwa kujiunga katika vikundi ili waweze kunufaika na fursa mbalimbali zinazotolewa na Mradi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Maendeleo (UNDP), unaolenga kuwaendeleza wachimbaji wadogo wa madini ya kimkakati, ikiwemo shaba. Wito huo umetolewa na Mhandisi Chacha Megewa kutoka Tume ya Madini, wakati wa utoaji wa elimu kwa wachimbaji katika mgodi wa Minosphere, maarufu kama mgodi wa Majuto, uliopo Kijiji cha Kitati. Akizungumza na wachimbaji hao, Mhandisi Megewa amesema kuwa ni muhimu wachimbaji kuunda vikundi vya angalau watu watano, ili waweze kufikiwa kwa urahisi kupitia huduma kama mafunzo, uunganishwaji na taasisi za kifedha, pamoja na upatikanaji wa mikopo inayolenga kuongeza tija katika shughuli zao za uchimbaji. “Uchimbaji salama na wenye tija unahitaji ushirikiano na uratibu mzuri. Kupitia vikundi, wachimbaji watapata nafasi kubwa zaidi ya kunufaika na fursa za kitaifa na ki...

TARURA YAENDELEA NA UKAGUZI WA BARABARA TEMEKE, YAELEZA MAFANIKIO YA MIRADI YA DMDP II

Image
Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) mkoa wa Dar es Salaam wamefanya ukaguzi wa ujenzi na matengenezo ya barabara katika mkoa huo unaolenga kuhakikisha miradi inakamilika kwa viwango na kwa wakati. Meneja wa TARURA mkoa wa Dar es Salaam, Mhandisi Geofrey Mkinga amesema kuwa, wametembelea wilaya ya Temeke ambapo walikagua barabara mbalimbali ikiwemo barabara ya kwa Diwani na zile zinazotekelezwa chini ya mradi wa Uendelezaji Jiji la Dar es Salaam awamu ya pili (DMDP). “Tumeona maendeleo mazuri kwenye utekelezaji, Mkandarasi yupo kazini na tunatarajia kujenga zaidi ya Km 7.2 katika eneo la makazi na biashara, ambapo magari makubwa na malori hupita mara kwa mara. Barabara zinajengwa kwa kiwango cha zege ili kukidhi mahitaji ya shughuli za kiuchumi zinazofanyika",  amesema Mkinga. Pia alitembelea barabara ya Yombo yenye urefu wa Km 1.6, ambapo ujenzi unaendelea kwa kiwango cha zege katika maeneo ya wazi pamoja na kipande cha mita 600 kinachojengwa kwa kushirikiana na Mani...

WACHIMBAJI WADOGO DODOMA WAPATIWA MAFUNZO YA USALAMA, AFYA NA UTUNZAJI WA MAZINGIRA MIGODINI*

Image
Mafunzo yanalenga kukuza uchimbaji salama, endelevu na wenye tija katika sekta ya madini ya shaba_ *Dodoma, Juni 27 2025* Wachimbaji wadogo kutoka migodi ya shaba iliyopo katika Mkoa wa Dodoma wamepatiwa mafunzo maalum kuhusu usalama mahali pa kazi, afya, utunzaji wa mazingira na usimamizi wa shughuli za uchimbaji.  Mafunzo hayo ni sehemu ya jitihada za kuimarisha uchimbaji salama na endelevu nchini. Mafunzo hayo yamewahusisha wachimbaji kutoka Mgodi wa Shengde uliopo Nala, Mgodi wa Hussein Pilly uliopo Tambi (Wilaya ya Mpwapwa) na Mgodi wa Canada uliopo Chamkoroma (Wilaya ya Kongwa) ambapo yamewezeshwa na Mpango wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa (UNDP) kwa kushirikiana na Tume ya Madini. Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mafunzo hayo, Mhandisi Chacha Megewa kutoka Tume ya Madini ameeleza kuwa ni muhimu kwa wachimbaji kufanya kazi katika mazingira salama kwa kutumia vifaa kinga kama kofia ngumu, reflekta, buti, gloves na barakoa (maski). "Ulipuaji wa baruti ni mojawapo ya shughuli ...

*DKT BITEKO MGENI RASMI NISHATI BONANZA 2025*

Image
📌 *Pamoja na kuimarisha afya za Watumishi; Linalenga kuhamasisha ushiriki wa Uchaguzi Mkuu 2025* 📌 *Ni la pili kufanyika tangu kuasisiwa na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko* Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati Mhe Dkt Doto Biteko anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika  Bonanza la Wizara ya Nishati na Taasisi zake litakalofanyika jumamosi Juni  28, 2025  jijini Dodoma. Akizungumzia maandalizi ya Bonanza  hilo, Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano Serikalini Wizara ya Nishati, Bi. Neema Mbuja amesema kuwa, Nishati Bonanza litafanyika kwenye Viwanja vya Jamhuri mjini Dodoma na kushirikisha taasisi zilizo chini ya Wizara ya Nishati na wadau kutoka Wizara nyingine. ‘’ Nipende kuchukua fursa hii kuzikaribisha taasisi zilizo chini ya  Wizara ya Nishati  kushiriki kikamilifu  bonanza ambalo linaleta fursa ya kufahamiana na kubadilishana mawazo baada ya muda wa kazi pamoja na  kufanya mazoezi ili kujenga afya." Amesema Mbuja Ameon...

TARURA KIGAMBONI YAANZA UJENZI WA BARABARA ZA LAMI KM 42 KUPITIA MRADI WA DMDP II

Image
Wakala ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) umeanza kutekeleza ujenzi wa barabara Km 42 kwa kiwango cha lami kupitia mradi wa Uendelezaji Jiji la Dar es Salaam Awamu ya Pili (DMDP II) katika Halmashauri ya Manispaa ya Kigamboni jijini Dar es Salaam. Hayo yameelezwa na Meneja wa TARURA Wilaya ya Kigamboni, Mhandisi Ismail Mafita ambapo amesema kuwa mpaka sasa wakandarasi watatu wapo “site” wanaendelea na ujenzi wa barabara Km 30 huku Km 10.2 zipo katika mchakato wa manunuzi. “Mpaka kufikia mwisho wa mwezi Juni mwaka huu zabuni zitatangazwa kwahiyo katika kipindi cha mwezi mmoja au miwili ijayo hizo Km 10 zitaanza kutekelezwa”, amesema Mhandisi Mafita.  Amesema kuwa tayari mradi wa DMDP II umeshaanza kuleta matokeo kwani barabara ambazo zilikuwa na changamoto zimeshaanza kufanyiwa kazi na wanatarajia mwakani mwezi Februari au Machi barabara zote Km 42 zitakuwa zimekamilika na kuleta matokeo makubwa katika manispaa ya kigamboni. “Jumla ya fedha zilizotengwa ni shilingi bilioni 1...

MIJI 11 MRADI WA TACTIC KUIMARISHA HUDUMA ZA USAFIRI

Image
#Waziri Mchengerwa akemea vikali Makandarasi wanao legalega Dodoma Waziri wa Nchi, Ofisi, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI) Mhe. Mohamed Mchengerwa amesema kuwa miradi ya TACTIC  katika miji 11 inaenda kuimarisha huduma za usafiri na usafirishaji . Mhe. Mchengerwa ameyasema leo jijini Dodoma wakati wa utiaji saini mikataba 12 ya utekelezaji wa miradi ya Uboreshaji wa Miundombinu ya Miji ya Tanzania (TACTIC) kwa miji ya Morogoro, Songea, Tanga, Korogwe, Babati, Shinyanga, Bukoba, Bariadi, Lindi, Iringa na Njombe. Amesema miradi hiyo pia inaenda kuimarisha huduma za kiuchumi kwa wananchi hususan upande wa mauzo na manunuzi kwa kuongeza thamani ya biashara nchini ambapo mazingira ufanyaji wa biashara kwenye ngazi za miji na majiji yanaenda kuboreshwa nchini. “Tunakusudia kuhakikisha kwamba utekelezaji wa miradi hii inatekelezwa kwa wakati, hatuna changamoto ya fedha kwahiyo sitegemei kuona mkandarasi ana legalega”. “Baadhi ya wakandarasi wakilipwa fedha wanapeleka kwenye ...

MBUNGE MAVUNDE AKABIDHI JENGO LA KUPUMZIKIA WANANCHI HOSPITAL YA RUFAA YA DODOMA*

Image
▪️RC Senyamule ampongeza kwa jengo na uanzishwaji wa ujenzi wa uzio ▪️Rais Samia apongezwa kwa maboresho makubwa ya huduma ya Afya ▪️Wananchi wamshukuru Mbunge Mavunde kwa utatuzi wa changamoto ya muda mrefu. Mbunge wa Jimbo la Dodoma Mjini Mh. Anthony Mavunde leo amekabidhi jengo la kupumzikia wananchi katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ambalo litasaidia kutatua changamoto ya wananchi wengi ambao hawakuwa na eneo lenye staha la kupumzika wakati wakiwa wanawahudumia wagonjwa wao. Hafla hiyo ya kukabidhi jengo hilo imeongozwa na Mkuu wa Mkoa wa Dodoma Mh. Rosemary S. Senyamule leo tarehe 25.06.2025. “Mh. Rais Dkt. Samia S. Hassan amefanya kazi kubwa ya maboresho ya vifaa na huduma ya Afya kwenye Hospitali hii ya Rufaa Dodoma. Kazi iliyofanywa na Mbunge Mavunde ni ya kuigwa mfano kwa kuwa ameunga mkono jitihada za Mh. Rais kwenye maboresho ya huduma za Afya. Jengo hili litasaidia sana  kuwafanya wananchi wa Dodoma na nje ya Dodoma kukaa kwenye mazingira mazuri na nadhifu,hivyo naagiza...