Kipeo Media ni chombo cha habari cha mtandaoni chenye kuleta taarifa za kina, sahihi, na kwa wakati. #KipeoOnlineMediaKilelechaHabariSahihinaBora.
RAIS DKT SAMIA AZINDUA KIWANDA CHA PAMBA MKOANI SIMIYU
Get link
Facebook
X
Pinterest
Email
Other Apps
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizindua Kiwanda cha kuchakata pamba cha Biosustain Tanzania Limited Meatu mkoani Simiyu tarehe 17 Juni, 2025.
Na,Agnes Mambo Tanga, Mkuu wa Mkoa wa Tanga, Balozi Dk Batilda Burian amesema maendeleo ya taifa hayawezi kupimwa kwa kiwango cha uwekezaji au ujenzi wa viwanda pekee, bali kwa namna serikali na jamii zinavyoweka fursa za usawa wa kijinsia katika ajira, hususan kwa watoto wa kike na wa kiume. Dk Burian ameyasema hayo alipokuwa akifungua maadhimisho ya nne ya Siku ya Kimataifa ya Wanawake katika Sekta ya Bahari yaliyofanyika jijini Tanga jana (Jumapili) Mei 18/2025. Akimnukuu mwanafalsafa maarufu Plato, aliyewahi kusema kuwa "Kilimo cha jamii yoyote ni jinsi inavyowathamini wanawake", Dk Burian alisisitiza kuwa taifa linapaswa kujipangia malengo ya kuhakikisha usawa wa kijinsia unatekelezwa kikamilifu. "Tusiache mwanamke abaki ufukweni bali tunataka aingie ndani ya bahari," alisema kwa msisitizo.. Alieleza kuwa licha ya juhudi zinazofanywa na serikali na wadau mbalimbali, sekta ya bahari bado inatawaliwa na wanaume, huku takwimu zikionyesha kuwa wanawake wanaofanya ...
Na,Agnes Mambo,Tanga. Jeshi la Polisi Mkoani Tanga limewakamata watuhumiwa 42 wanaohusishwa na matukio mbalimbali ya uporaji, umiliki wa dawa za kulevya, pamoja na pikipiki zisizosajiliwa na mafuta yanayodhaniwa kuwa ya magendo. Operesheni hiyo iliyoanza Juni 15, ni juhudi mpya za vyombo vya dola kusafisha jiji dhidi ya ongezeko la vitendo vya kihalifu. Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Jumanne, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Almachius Muchunguzi, alisema watuhumiwa hao walikamatwa katika operesheni maalum inayoendelea inayolenga maeneo yenye viashiria vya uhalifu jijini. Miongoni mwa waliokamatwa ni watu watano wanaoshukiwa kumvamia na kumpora kwa nguvu Katwibu Siraji, mwalimu wa Shule ya Sekondari Postal. Watuhumiwa hao wanadaiwa kumpiga na kuiba simu ya mkononi ya mwalimu huyo, tukio lililozua taharuki miongoni mwa wananchi na kuongeza shinikizo kwa polisi kuchukua hatua. Kamanda Muchunguzi alikiri kuwepo kwa ongezeko la visa v...
OR-TAMISEMI Serikali kupitia Programu Jumuishi ya Taifa ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto (PJT-MMMAM) imefanikiwa kuanzisha vituo 206 vya kijamii vya kulelea watoto wadogo mchana na kusajili vituo binafsi 4,178 nchi nzima tangu mwaka 2021. Akizungumza kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Mhe. Mohamed Mchengerwa, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhe. Said Mtanda, amesema vituo hivyo vinahudumia jumla ya watoto 11,675 huku vya binafsi vikihudumia watoto 6,154. Aidha, jumla ya walezi 445 wamepatiwa mafunzo ya malezi na makuzi ili kuhakikisha utoaji bora wa huduma katika vituo hivyo. Mtanda alisisitiza kuwa uwekezaji katika malezi ya awali ni msingi wa kukuza rasilimali watu yenye tija kwa familia na taifa kwa ujumla. Kwa upande wake, Mwakilishi wa Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Bw. Sebastian Kitiku, amesema mkutano wa tathmini wa siku mbili unawaleta pamoja Maafisa Lishe kutoka Tanzania Bara na Zanzibar pamoja na wadau wa maendeleo ili kujadili maf...
Comments
Post a Comment