WAZIRI MKUU ATEMBELEA KITUO CHA MALEZI YA WATOTO, SANGANIGWA, KIGOMA*


WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa leo Juni 13, 2025 ametembelea kituo cha kulea watoto wenye uhitaji cha Sanganigwa kilichopo mjini Kigoma, kinachosimamiwa na Kanisa Katoliki jimbo la Kigoma.

Akizungumza na watoto na walezi wa kituo hicho, Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa Serikali inayoongozwa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inatambua mchango wa madhehebu ya dini katika kuwalea kimwili na kiroho watoto wenye mahitaji maalum nchini.

“Kwa niaba ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, ninalishukuru kanisa katoliki jimbo la Kigoma, mtu mmoja mmoja na taasisi mbalimbali ambazo zimekuwa msaada mkubwa kwa Serikali katika kuwalea watoto wetu, hakika mnafanya jambo kubwa na lakumpenda Mungu na wanadamu”

Akisoma taarifa ya kituo hicho kwa Waziri Mkuu, Mkurugenzi wa Kituo hicho Keneth Hageze amesema kuwa kilianzishwa mwaka 1995 na mpaka sasa kimehudumia watoto 1309.

Mheshimiwa Majaliwa alitoa Mchele, Maharage, Mafuta, Sukari pamoja na Taulo za kike.




 

Comments

Popular posts from this blog

HATMA YA TAIFA IPO KATIKA USAWA WA KIJINSIA, SIO VIWANDA PEKEE.

MSAKO MKALI KUREJESHA HALI ya USALAMA TANGA, WATUHUMIWA 42 WAKAMATWA

PJT-MMMAM YAWEZESHA UANZISHWAJI WA VITUO 206 VYA MALEZI YA WATOTO WADOGO