MHE. KITANDULA ATEMBELEA BANDA LA NCAA KATIKA MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA


Mhe. Naibu Waziri wa Mali Asili na utalii Mhe. Dustan Kitandula (Mb) leo Juni 20, 2025 ametembelea banda la NCAA lililopo ndani ya Banda la Wizara ya Mali asili na Utalii kwenye Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma yanayoendelea jijini Dodoma katika Viwanja vya Chinangali Park.

Akiwa ndani ya Banda hilo, Mhe. Kitandula ametoa wito kwa NCAA kuendelea kutoa Elimu kwa umma kuhusiana na jamii inayoishi ndani ya Eneo la Hifadhi ya Ngorongoro kwa kulezea historia  na asili halisi ya jamii hiyo.

Aidha, Naibu Waziri amewahimiza wananchi kujitokeza kwa wingi kutembelea banda hilo la Wizara ya Maliasili na Utalii ili kupata elimu kuhusu shughuli za uhifadhi pamoja na fursa mbalimbali za uwekezaji zinazopatikana katika sekta ya utalii.

Maadhimisho ya Wiki ya Utumishi wa Umma kwa mwaka huu yalianza rasmi Juni 16, 2025, na yanatarajiwa kufikia kilele chake Juni 23, 2025, yakihusisha taasisi mbalimbali za umma zikiwemo zile zilizopo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii.




 

Comments

Popular posts from this blog

HATMA YA TAIFA IPO KATIKA USAWA WA KIJINSIA, SIO VIWANDA PEKEE.

MSAKO MKALI KUREJESHA HALI ya USALAMA TANGA, WATUHUMIWA 42 WAKAMATWA

PJT-MMMAM YAWEZESHA UANZISHWAJI WA VITUO 206 VYA MALEZI YA WATOTO WADOGO