WIZARA YA NISHATI NA TAASISI ZAKE YASHIRIKI MAADHIMISHO YA WIKI YA UTUMISHI WA UMMA DODOMA*


Wizara ya Nishati na taasisi zilizo chini yake inashiriki Maadhimisho ya Kitaifa ya Wiki ya Utumishi wa Umma ambayo yameanza Juni 16, 2025 katika viwanja vya Chinangali, Jijini Dodoma.

Maadhimisho hayo yamebebwa na kaulimbiu isemayo "Himiza Matumizi ya Mifumo ya Kidijiti Kuongeza Upatikanaji wa Taarifa na Kuchagiza Uwajibikaji", 

Watalaam wa Wizara pamoja na kueleza mafanikio yaliyofikiwa katika Sekta ya Nishati ikiwemo ukamilishaji wa mradi wa umeme wa Julius Nyerere na usambazaji wa umeme vijijini, wanatoa elimu  kwa njia mbalimbali ikiwemo machapisho na vitendo kuhusu ajenda ya kitaifa ya  utekelezaji wa Mkakati wa Nishati Safi ya kupikia.

Taasisi za Wizara ya Nishati zinazoshiriki maadhimisho hayo ni Shirika la Umeme Tanzania ( TANESCO), Mamlaka ya Udhibiti wa Mkondo wa Juu wa Petroli ( PURA),  Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA), Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania ( TPDC), Wakala wa Nishati Vijijini ( REA) na Wakala wa Uagizaji wa Mafuta kwa Pamoja (PBPA).




 

Comments

Popular posts from this blog

HIFADHI YA NGORONGORO YASHIRIKISHA WATALII UZINDUZI WA WIKI YA HUDUMA KWA WATEJA.

NMB Same Yachochea Ari ya Mafanikio kwa Wanafunzi, Yasema “Bidii, Nidhamu na Malengo” Ndio Siri ya Ushindi

ANNE KILANGO AZINDUA KAMPENI SAME MASHARIKI KWA KISHINDO