OFISI YA WAZIRI MKUU-TAMISEMI KUSHUGHULIKIA WATUMISHI WAZEMBE



Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM-TAMISEMI) anayeshughulikia Elimu, Mhe. Reuben Kwagilwa, amesisitiza kuwa ofisi hiyo itaendelea kuchukua hatua kwa watumishi wazembe na wanaotumia vibaya fedha za Serikali. 

Akizungumza wakati wa ziara ya kikazi ya Waziri Mkuu, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba mkoani Songwe, Mhe. Kwagilwa ameeleza kwamba ofisi hiyo itafika katika Halmashauri zote nchini ili kuhakikisha watumishi wanaofuja fedha za Serikali katika miradi ya maendeleo wanawajibishwa ipasavyo. 

“Ofisi ya Waziri Mkuu-TAMISEMI inasisitiza dhamira yake ya kuhakikisha kwamba fedha za Serikali zinatumiwa kwa ufanisi na kwa manufaa ya maendeleo ya jamii,” aliongeza Mhe. Kwagilwa.




Comments

Popular posts from this blog

HIFADHI YA NGORONGORO YASHIRIKISHA WATALII UZINDUZI WA WIKI YA HUDUMA KWA WATEJA.

NMB Same Yachochea Ari ya Mafanikio kwa Wanafunzi, Yasema “Bidii, Nidhamu na Malengo” Ndio Siri ya Ushindi

ANNE KILANGO AZINDUA KAMPENI SAME MASHARIKI KWA KISHINDO