VIJANA MTWARA WATAKA FURSA
Na. OR – MV, Mtwara Vijana wa mkoa wa Mtwara wamesema wanahitaji Serikali iwasaidie kuweka mazingira wezeshi ili fursa za kiuchumi zilizopo ziwasaidie kuzalisha ajira na kudumisha amani ikiwa ni matunda ya kuanzishwa wizara ya vijana kwa mara ya kwanza nchini. Akizungumza kwa nyakati tofauti wakati na vijana, Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Maendeleo ya Vijana na mbunge wa Mtwara Mjini Joel Nanauka (29 Novemba 2025) mjini Mtwara alisema Serikali itatumia muda mwingi kutafuta fursa za maendeleo kwa vijana badala ya kudhibiti vijana. Waziri wa Maendeleo ya Vijana Joel Nanauka aliwaeleza vijana kuwa dhmaira ya kuundwa wizara hiyo ni kutekeleza maono ya Rais Samia Suluhu Hassan ya kuona mawazo na fikra za vijana nchini zinasikika ili kutatua changamoto zao. Nanauka aliongeza kusema katika kuhakikisha vijana wanapata mitaji na kuwa na uhakika wa kipato amekusidia kuanzisha mfuko maalum wa vijana (Saccos) waendesha pikipiki na akina mama wajasiliamali ambapo atachangia mfuko uwe na uwezo w...