MABAKI YA MWILI WA MTANZANIA JOSHUA MOLLEL YAWASILI NCHINI TANZANIA



Mabaki ya mwili wa Kijana Joshua Mollel aliyeuwawa nchini Israel na wapiganaji wa HAMAS Oktoba 07, 2023 yamewasili leo Novemba 19, 2025 katika kiwanja cha Ndege cha kimataifa cha Kilimanjaro (KIA).

Mabaki ya mwili huo yamepokelewa na Ujumbe wa Serikali ya Jamhuri ya  Muungano wa Tanzania ukiongozwa na  Naibu katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Balozi Said Shaib Mussa na Balozi Silima Haji Kombo. 

Mabaki ya Kijana Joshua Mollel yanatarajiwa kuzikwa   kesho  Novemba 20,  2025 mtaa wa Njiro, katika kata Orkesumet Wilaya ya Simanjiro,  Mkoani Manyara.




Comments

Popular posts from this blog

HATMA YA TAIFA IPO KATIKA USAWA WA KIJINSIA, SIO VIWANDA PEKEE.

MSAKO MKALI KUREJESHA HALI ya USALAMA TANGA, WATUHUMIWA 42 WAKAMATWA

PJT-MMMAM YAWEZESHA UANZISHWAJI WA VITUO 206 VYA MALEZI YA WATOTO WADOGO