MELI KUBWA YA MZIGO KUTOKA IRAN YATIA NANGA BANDARI YA TANGA.



Na,Agnes Mambo,Tanga..

Mkuu wa mkoa wa Tanga amesema wataendelea kujenga mahusiano mazuri ya kibiashara na nchi ya Irani Kwa kufanyabiasha ikiwemo kubadilishana bidhaa Kwa bei nafuu Kwa kuanzisha VIWANDA vidogo vidogo vya machine za uzalishaji bidhaa mbalimbali.

Aidha Mkuu wa mkoa wa Tanga Balozi Dkt Batilda Burian ameendelea kuishukuru Serikali ya awamu ya sita Kwa maboresho ya Bandari ya Tanga yameendelea kuzaa matunda kutokana na kupokea Meli kubwa za mizigo mara kwa mara na mapato ya kiuchumi kuongezeka mara dufu.

Pongezi hizo amezitoa Novemba 28 akiwa katika Bandari ya Tanga baada kupokea Meli kubwa ya mizigo yenye tani elfu 13 kutoka nchini Irani iliyobeba makontena 463 kati ya hayo makontena 261 mizigo ya ndani na makontena 182 ambayo yanasafirishwa kwenda nchi za Afika Mashariki.


Kwa upande wake kaimu Meneja wa Bandari,Peter Milanzi amesema Kwa mara ya kwanza Bandari ya Tanga kuandika historia ya kupokea Meli kubwa ya Moja Kwa Moja kutoka nchini Irani iliyofahamika Kwa Jina la Uleni Kontena MV Pania.

Amesema tunayofuraha kubwa kutokana kwamba tumezoea kupokea Meli ndogo lakini hivi sasa tunapokea Meli kubwa hivyo tunashukuru rais Dkt Samia Kwa kuwekeza fedha nyingi kuboresha Bandari ya Tanga na kuandika histori ya kuongezeka Kwa mapato.

Amesema Meli hii imechukuwa siku nane kutoka Irani kuja Tanga Moja Kwa Moja.




Comments

Popular posts from this blog

HATMA YA TAIFA IPO KATIKA USAWA WA KIJINSIA, SIO VIWANDA PEKEE.

MSAKO MKALI KUREJESHA HALI ya USALAMA TANGA, WATUHUMIWA 42 WAKAMATWA

PJT-MMMAM YAWEZESHA UANZISHWAJI WA VITUO 206 VYA MALEZI YA WATOTO WADOGO