MAKAMU WA RAIS AFANYA MAZUNGUMZO NA MAKAMU WA RAIS WA JAMHURI YA ZIMBABWE*

*TANZANIA NA ZIMBABWE ZAKUBALIANA KUENDELEZA UHUSIANO* Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amekutana na kufanya mazungumzo na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Zimbabwe Mhe. Kanali Mstaafu Kembo Campbell Mohadi, Mazungumzo yaliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam wakati wa ziara ya siku mbili ya Makamu wa Rais wa Zimbabwe hapa nchini. Katika siku ya kwanza ya Ziara ya Makamu wa Rais Zimbabwe, viongozi hao wameongoza Ujumbe wa Tanzania na Jamhuri ya Zimbabwe katika mazungumzo rasmi ambayo yamelenga namna ya kukuza uhusiano na ushirikiano kati ya mataifa hayo mawili. Mazungumzo hayo yamegusia zaidi urafiki wa muda mrefu wa kihistoria baina ya Tanzania na Zimbabwe tangu enzi za harakati za ukombozi wa Taifa la Zimbabwe, ambapo Tanzania chini ya uongozi wa Baba wa Taifa, Hayati Mwalimu Julius Kambarage Nyerere ilitoa msaada wa hali na mali kwa wapigania uhuru wa Zimbabwe. Tanzania na Zimbabwe zimekubaliana kuendeleza uhusiano uliopo pamoja na kutunza histor...