SEKENKEONE - SHELUI, WILAYA YA IRAMBA KUMEKUCHA KONGAMANO LA WACHIMBAJI WADOGO KANDA YA KATI.


Kongamano hilo litakaloambatana na matembezi ya Amani, linalenga kumpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa mafanikio yaliyopatikana katika Sekta ya Madini katika kipindi cha miaka Minne.

Katika miaka hii minne Sekta ya Uchimbaji Mdogo imekua huku mazingira wezeshi yaliyowekwa na Serikali ikiwemo kupatiwa maeneo ya kuchimba, uwepo wa masoko ya madini nchini na masuala mengine  yamechangia  ukuaji wa shughuli za uchimbaji mdogo  ambapo hivi sasa zinachangia asilimia 40 ya makusanyo ya Maduhuli ya Serikali.

Mgeni rasmi ni Waziri wa Madini Mhe. Anthony Mavunde na litarushwa mbashara kupitia TBC1

*Vision 2030:

Madini ni Maisha na Utajiri*




 

Comments

Popular posts from this blog

HATMA YA TAIFA IPO KATIKA USAWA WA KIJINSIA, SIO VIWANDA PEKEE.

MSAKO MKALI KUREJESHA HALI ya USALAMA TANGA, WATUHUMIWA 42 WAKAMATWA

PJT-MMMAM YAWEZESHA UANZISHWAJI WA VITUO 206 VYA MALEZI YA WATOTO WADOGO