DKT. BITEKO AOMBA KURA YA NDIYO KWA WAJUMBE BUKOMBE

Dkt. Biteko amesema hayo Agosti 2, 2025 kwa nyakati tofauti wakati akiomba kura kwa wajumbe wa Chama cha Mapinduzi wa Kata za Lyambamgongo, Uyovu, Bugelenga, Katome, Igulwa na Runzewe Mashariki zilizopo katika Jimbo la Bukombe.
" Mimi na viongozi wenzangu wakiwemo wa vijiji na madiwani ukianzia sekta ya Nishati tumesambaza umeme kila mahali, Sekta ya miundombinu tumeongeza mtandao wa barabara kutoka km 259 hadi km 1,445 na Sekta ya Elimu tunaongoza kwa kuwa na shule nyingi za Msingi na Sekondari tofauti na ilivyokuwa Mwaka 2015 hatukuwa na shule ya sekondari ya upili hata moja lakini mwaka 2025 tunazo shule TANO, Kwa upande wa sekta ya afya tumepata miradi mbalimbali na fedha nyingi za kuboresha huduma za afya katika wilaya yetu ya Bukombe”.

Comments
Post a Comment