MAMLAKA YA HIFADHI YA NGORONGORO NCAA INASHIRIKI MAONESHO YA NANE NANE KANDA YA KASKAZINI ARUSHA


Mamlaka ya Hifadhi ya eneo la Ngorongoro (NCAA) inashiriki Maonesho ya Wakulima NaneNane Kanda ya Kaskazini katika viwanja vya Themi Njiro Arusha, Viwanja vya Nzuguni Jijini Dodoma na Uwanja wa John Mwakangale Jijini Mbeya  kwa ajili ya kutoa elimu kwa Watanzania kuhusu vivutio vya utalii, urithi wa Utamaduni na Mambo Kale,  Uhifadhi shirikishi, maendeleo ya jamii pamoja na fursa za uwekezaji zinazopatikana katika hifadhi ya Ngorongoro.

Tembelea banda letu la NCAA uweze kujua mengi kuhusu hifadhi ya Ngorongoro ambayo ni kivutio namba moja cha utalii barani Afrika na  moja ya chaguo bora la wageni wa Safari waliotembelea kwa mujibu wa mtandao wa TripAdvisor 

Maonesho ya NaneNane yalianza rasmi Agosti 01, 2025  na kaulimbiu ya mwaka huu ni “Chagua viongozi bora kwa maendeleo endelevu ya kilimo,mifugo na uvuvi 2025” na yanatarajiwa kutamatika mnamo Agosti 08, 2025.




 

Comments

Popular posts from this blog

HATMA YA TAIFA IPO KATIKA USAWA WA KIJINSIA, SIO VIWANDA PEKEE.

MSAKO MKALI KUREJESHA HALI ya USALAMA TANGA, WATUHUMIWA 42 WAKAMATWA

PJT-MMMAM YAWEZESHA UANZISHWAJI WA VITUO 206 VYA MALEZI YA WATOTO WADOGO