Mhe. NDEJEMBI AKUTANA NA CHAMA CHA WAAGIZAJI NA WASAMBAZAJI WA MAFUTA (TAOMAC)



Waziri wa Nishati, Mhe. Deogratius Ndejembi, amekutana na kufanya mazungumzo na Chama cha Waagizaji na Wasambazaji wa Mafuta Tanzania (TAOMAC) kwa lengo la kuboresha na kukuza sekta ya mafuta nchini pamoja na kuimarisha ushirikiano kati ya Serikali na wadau wa sekta hiyo.

Kikao hicho kimefanyika leo, Machi 5, katika Ofisi Ndogo za Wizara ya Nishati zilizopo jijini Dar es Salaam.

Katika Kikao hicho wamejadili masuala mbalimbali yanayolenga kuimarisha usimamizi, ufanisi na maendeleo ya sekta ya mafuta nchini kwa manufaa ya uchumi na wananchi kwa ujumla.

Kikao hicho kimehudhuriwa na Kamishna wa Mafuta kutoka Wizara ya Nishati, Bw. Goodluck Shirima; Mtendaji Mkuu wa PBPA, Bw. Erasto Simon; Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Dkt. James Mwainyekule; pamoja na viongozi na wanachama wa TAOMAC.




Comments

Popular posts from this blog

HATMA YA TAIFA IPO KATIKA USAWA WA KIJINSIA, SIO VIWANDA PEKEE.

MSAKO MKALI KUREJESHA HALI ya USALAMA TANGA, WATUHUMIWA 42 WAKAMATWA

PJT-MMMAM YAWEZESHA UANZISHWAJI WA VITUO 206 VYA MALEZI YA WATOTO WADOGO