WAPIGA KURA WAJITOKEZA KWA WINGI KATA YA KIRUMBA, ILEMELA – MWANZA



Zoezi la kupiga kura linaendelea kwa hali ya utulivu katika Kata ya Kirumba, Halmashauri ya Ilemela, jijini Mwanza, huku wananchi wakijitokeza kwa wingi kutekeleza haki yao ya kikatiba.

Wananchi wameonekana wakiwa katika mistari wakiingia vituoni mapema asubuhi, wakisubiri kwa utulivu nafasi yao ya kupiga kura. Maafisa wa Tume ya Uchaguzi wamesema maandalizi yamekuwa mazuri na vifaa vyote vya kupigia kura vimefika kwa wakati.

Wamewataka wapiga kura kuendelea kujitokeza kwa amani na kufuata maelekezo yanayotolewa na wasimamizi wa vituo, ili kuhakikisha zoezi hilo muhimu kwa demokrasia ya nchi linafanikiwa kwa utulivu na uwazi.



Comments

Popular posts from this blog

HIFADHI YA NGORONGORO YASHIRIKISHA WATALII UZINDUZI WA WIKI YA HUDUMA KWA WATEJA.

NMB Same Yachochea Ari ya Mafanikio kwa Wanafunzi, Yasema “Bidii, Nidhamu na Malengo” Ndio Siri ya Ushindi

ANNE KILANGO AZINDUA KAMPENI SAME MASHARIKI KWA KISHINDO