REA YAPAMBA MAONESHO YA KITAIFA YA TEKNOLOJIA YA MADINI GEITA*



*📌Yaendelea kusambaza majiko ya gesi na  majiko banifu kwa bei ya ruzuku*

*📌Wananchi waaswa kutembelea banda la REA kupewa elimu ya miradi ya umeme kwenye vitongoji na nishati safi*

*📌Geita waipongeza REA kwa utekelezaji wa miradi ya nishati safi ya kupikia*

📍Geita

Wakala wa Nishati Vijijini (REA), imekuwa kivutio pekee kwa taasisi za Serikali zinazoshiriki katika Maonesho ya Nane ya Kitaifa ya Teknolojia ya Madini yanayofanyika katika viwanja vya Dkt. Samia Suluhu Hassan mkoani Geita. 

Ushiriki wa REA katika maonesho hayo umevutia wananchi wengi kutembelea banda la Wakala ambapo wataalam kutoka REA wanaendelea kutoa elimu ya miradi mbalimbali ya REA inayotekelezwa hapa nchini kwa mafanikio pamoja kuhamasisha matumizi ya nishati safi ya kupikia kwa kusambaza na kuuza majiko banifu kwa bei ya ruzuku na majiko ya gesi.


Comments

Popular posts from this blog

HATMA YA TAIFA IPO KATIKA USAWA WA KIJINSIA, SIO VIWANDA PEKEE.

MSAKO MKALI KUREJESHA HALI ya USALAMA TANGA, WATUHUMIWA 42 WAKAMATWA

PJT-MMMAM YAWEZESHA UANZISHWAJI WA VITUO 206 VYA MALEZI YA WATOTO WADOGO